RAIS na mwenyekiti wa
serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Dkt, Husein Ally Mwinyi natarajiwa kuwa mgeni
Rasmi kwenye maadhimisho ya ubunifu na
mashindano ya sayansi kitaifa
Akizungumza na waandishi
wa vyombo mbalimbali vya habari jijini Dodoma Waziri wa Elimu, Sayansi
na Teknolojia (MAKISATU)2022 Prof Adolf Mkenda amesema kuwa Dkt, atafungua
mashindano hayo mei 16 mwaka huu
Mkenda amesema
maadhimisho hayo yanalenga pamoja na mambo mengine kuibua, kutambua na kuendeleza
jitihada zinazofanywa na wabunifu wa kitanzania na kuhamasisha matumizi ya
teknolojia na ubunifu wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii
Aidha amesema maadhimisho
hayo ya wiki ya kitaifa ya ubunifu yanatoa fursa kwa wabunifu/wagunduzi
kujitangaza na kujulikana kwa wawekezaji, watumiaji wa bidhaa zao na wadau
wengine ndani nan je ya nchi
Ameongeza kuwa wiki ya
ubunifu ni mkakati wa serikali way a awamu ya 6 wa kuhamsisha matumizi ya
Sayansi, teknolojia na ubunifu kama nyenzo ya kutatua changamoto za kiuchumi na
kijamii
Amesema tayari
maadhimisho hayo kimkoa yamesaanza katika mikoa 16 tangu aprl 27 ambapo kitaifa
yatarajiwa kuanza mei 15 mwaka huu katika uwanja wa jamhuri jijini Dodoma na
kwamba kilele kitakuwa mei 19 yakifungwa na makamu wa rais Philip Mipango