Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Amon Mpanju amekitaka Kikosi Kazi cha
kuratibu ukusanyaji maoni kuhusu Mkakati wa Uendelevu wa NGOs kushirikiana na
wadau nje ya Sekta hiyo kupata maoni yatakayosaidia kuwa na Mkakati wenye tija
kwa maendeleo ya NGOs.
mpanju ameyasema hayo Mei 14, 2022 jijini Mbeya
wakati akifungua kikao cha wadau wa NGOs kwa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini
kilicholenga ukusanyaji maoni juu ya Mkakati wa Uendelevu wa NGOs nchini.
Aliongeza kuwa nia ya Serikali ni kuhakikisha NGOs
zinakuwa na mazingira mazuri ya kushiriki kuunga mkono juhudi za Serikali
katika kuhudumua jamii na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
Mpanju alisema ili kuwa na mkakati wenye tija
ni muhimu wadau wote wakashirikishwa katika kutoa maoni yao ili kuwa na
uwanda wa mawazo na kuwa na Mkakati shirikishi.
"Pamoja na yote mtakayoyatekeleza
hakikisheni ili tuwe na mpango kazi unaoakisi uhalisia mkutane pia na wadau wa
ambao wapo nje ya Sekta yenu ya NGOs "alisema Mpanju
Mpanju alisema lengo la mkakati huo wa
kitaifa ni kuwa na dira ya namna ya NGOs kuweza kujitegemea na kuwa na
uendelevu wa shughuli wanazofanya hivyo amewataka Wasajili wasaidizi wa Mikoa
na Wilaya ambao ni Maafisa Maendeleo ya Jamii kushiriki katika kuhakikisha NGOs
hazilundikani katika eneo moja zikitoa huduma zinazofanana kwa watu wa eneo
moja.
"Zoezi hili ni kwa ajili yenu kupata
fursa ya kutoa maoni kwa niaba ya NGOs na kwa maslahi ya wananchi mnao
wahudumia nyie ni wadau muhimu sana mnaofanya kazi njema, kazi ya kutukuka,
kuleta ukombozi, elimu na kuwainua wananchi ambao ni wanufaika kupitia kazi
zenu" alisema Mpanju.
Aidha alibainisha kuwa Serikali inatambua
mchango wa NGOs kwani sekta hiyo imesaidia kuongeza ajira kwa wananchi na pia
kuunga mkono juhudi za Serikali katika kupambana na ukatili dhidi ya
wanawake,watoto na kiketabusawa wa Kijinsia katika jamii.
Wakati huo huo Naibu Katibu Mkuu Amon Mpanju
ametumua fursa hiyo kuhumiza familia kuwa na Utamaduni wa kuzungumza
na kuzingatia malezi na makuzi bora ya Watoto katika jamii kuelekea
Siku ya Kimataifa ya Familia inayofanyika kila Mei 15 na .
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha
kuratibu ukusanyaji maoni juu ya Mkakati wa Uendelevu wa Mashirika Yasiyo ya
Kiserikali Nensia Mahenge alisema Mkakati huo wa Uendelevu wa Mashirika ya
itasaidia Mashirika hayo kuweka kujiendesha na kutekeleza majukumu yao hata kusipokuwepo
na ufadhili kutoka kwa wadau wa maendeleo.
"Tusikie maoni mapendekezo mawazo ya
wadau wote kuhusu kuendelea kutoa huduma kwa jamii bila kuathiriwa na sababu
mbalimbali ikiwemo ufadhili wa nje, tumeshuhudia wakati wa majanga mbalimbali,
baadhi ya Mashirika kushindwa kujiendesha" alisisitiza Nensia.
Naye Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya
Donald Bombo alisema Mkoa wa Mbeya unashirikia karibu na Mashirika Yasiyo ya
Kiserikali katika kutekeleza miradi mbalimbali na huduma kwa wananchi hasa katika
maeneo ya vijijini.
Nao baadhi ya wadau kutoka Mashirika Yasiyo ya
Kiserikali kutoka Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini walisema Mkakati huo utasaidia
NGOs kuwa na uwezo wa kuendelea kutekeleza majukumu yao kupitia miradi na
utoaji wa huduma kwa wananchi hivyo kupunguza utegemezi kutoka kwa wafadhili.