BANDA MEDIA BLOG

No title

MAMLAKA ya Elimu Tanzania (TEA) Yashiriki wiki ya Ubunifu huku ikijivunia kuwawezesha watanzania Elfu 32 
Mmoja wa wanufaika wa mfuko wa kuendeleza ujuzi (SDF), Eunice Kavishe ambaye ni fundi wa kutengeza simu akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari hawapo pichani (PICHA ZOTE NA JOHN BANDA)

Afsa habari na mawasiliano wa TEA Eliafile Solla, akiwa pamoja na Mbunifu Frank Kisamo, wakiwaonyesha waandishi wa habari Mbolea hai inayotengenezwa kwa kutumia kinyesi cha wanyama na mabaki ya chakula ambapo mbunifu huyo aliibuni kwa kuwezeshwa na mfuko wa kuendeleza ujuzi (SDF)
Afsa habari na mawasiliano wa TEA Eliafile Solla akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari, katika uwanja wa jamhuri jijini Dodoma, kunakoonyeshwa kazi mbalimbali za ubunifu zinazofanywa na watanzania

Mjasiliamali Ester Shebe akimhudumia mteja Wine, iliyotengenezwa kwa malighafi ya Uyoga ambao pia anautumia kutengenezea keki,achali na biskuti, mwanadada huyo anawezeshwa na mfuko wa kuendeleza ujuzi (SDF)

NA JOHN BANDA, DODOMA

MAMLAKA ya Elimu Tanzania (TEA) Imewashauri watanzania kuwa wabunifu ili kuleta maendeleo endelevu nchini hali itakayowafanya kujiinua kiuchumi na kuondokana na umasikini 

Pia,  TEA imefanikiwa kuwawezesha watanzania zaidi ya 32 elfu chini ya Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF) kwa kuwapatia mafunzo ya ujasiriliamali yakiwemo ya ubunifu katika sekta sita

Kauli hiyo imetolewa na Afisa habari na Uhusiano  wa Mamlaka ya Elimu Tanzania(TEA) Bi Eliafile Solla wakati akizungumza na waandishi wa Habari katika Wiki ya Ubunifu Kitaifa 2022 (MAKISATU) Jijini Dodoma.

Aidha Bi Eliafile amesema Ubunifu ni sehemu ya kila mtu ikiwa ataamua kujishughulisha bila kukata tamaa na kuongeza ujuzi kwa kujiunga na mafunzo yanayotolewa na ruzuku ya mfuko wa kuendeleza ujuzi (SDF).

Eliafile ameongeza kuwa zaidi  ya watu elfu 32 nchini  wamenufaika kwa kuwezeshwa kimafunzo na ubunifu wakiwezeshwa na mfuko wa kuendeleza ujuzi (SDF), ruzuku iliyojikita katika sekta sita za kipaumbele ambazo ni uchukuzi, nishati, ujenzi, utalii,na huduma za ukarimu, Teknojia ya habari TEHAMA pamoja kilimo biashara.

Maonyesho ya wiki ya wabunifu MAKISATU mwaka huu yana kauli mbiu   isemayo "Ubunifu kwa Maendeleo endelevu".

Kwa upande wake mnufaika wa mafunzo ya mfuko wa kuendeleza ujuzi (SDF)' Malkia wa nguvu 2022 kilimo na Bishara Esther Shebe,  ambaye Aliacha kazi ya uuguzi tangu mwaka 2018 na kuamua kuwa mjasiriamali  amesema wanaishukuru serikali kwa kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali kwani kupitia mafunzo hayo wamejikwamua na umaskini.

Hata hivyo Esther  amewashauri wanawake na vijana kujishughulisha kwa kufanya kazi zinazowaingizia kipato bila uoga ili  waepukane na  utegemezi.

 

 

 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG