BANDA MEDIA BLOG

No title


DRC yazindua kituo kikubwa cha Kifedha Kinshasa kilichojengwa na kampuni ya Kituruki


 Katika jitihada za kukuza uchumi wa nchi kupitia rasimali zake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imefungua majengo ya kituo cha kifedha katika jiji lake la Kinshasa mnamo Disemba 19, 2023.

Kituo cha Kifedha cha Kinshasa ni kitovu cha kifedha kilichoko kimkakati katika wilaya ya Gombe jijini Kinshasa, katika eneo la magharibi mwa DRC.

Ujenzi wa jumla ya majengo 11 katika eneo la mita za mraba 165,000 ulioanza mnamo mwezi Februari mwaka 2022 umekamilika mwezi Disemba mwaka 2023. Eneo hili kubwa linakifanya kituo hiki kuwa kituo kikubwa zaidi cha kifedha nchini humo.

Wahandishi wa Uturuki ndio waliojenga mradi huo kwa muda mfupi. Ubunifu wa majengo hayo ya kisasa na ujenzi wake umefanywa na kampuni ya ujenzi ya Kituruki Milvest, kampuni tanzu ya Miller Holding.

Tangu jiwe la msingi liwekwe mwezi Juni mwaka 2022, ni takriban mwaka mmoja na nusu umewatosha wahandishi hao kumaliza mradi huu mkubwa nchini. Na Jumla ya wafanya kazi 3000 ikiwa Wakongo 1500 na Waturuki 1500 wamefanya kazi kwenye ujenzi huu.

Ndoto ya Tshisekedi imetimia

Ikiwa ni moja ya ndoto za rais Felix Tshisekedi kuijenga DRC na kuiweka katika nafasi ya kipekee si barani Afrika tu bali hata duniani imefikiwa baada ya kufungua kituo hicho cha kifedha.

Ujenzi huu umeigharimu DRC takriban dola za kimarekani 290 hadi kukamilika. Kituo kitakapoanza kazi rasmi, watu 5000 wanatarajiwa kufanya kazi ambao watahudumu raia wa DRC kwenye sekta ya fedha.

Kuna nini hapa kwenye kituo cha kifedha?

Kituo hiki kinajumuisha taasisi muhimu kama vile Wizara ya Fedha na Bajeti, Kurugenzi Kuu, Mkaguzi Mkuu wa Fedha, Sekretarieti Kuu ya Fedha na Benki ya Maendeleo. Kwa ujumla kuna taasisi 9 zinazohusiana na Wizara ya Fedha ya nchi hiyo.

Kinasimamiwa na shirika la kibiashara la Hazina ya Uwekezaji inayomilikiwa na serikali, ambayo inasimamia mali isiyohamishika kama vile vituo vya kifedha na mikutano.

Jengo la ofisi za kikazi lenye ghorofa 19 ndio refu zaidi, ndani ya eneo hili pia kuna jengo la hoteli ambao ni uwekezaji binafsi wa kampuni ya Milvest.

Katika sifa za kipekee za kituo hiki ni kwamba ndani yake kuna ukumbi wa mikutano wa kisasa wenye uwezo wa kupokea watu 3000 kwa wakati mmoja na kuufanya kuwa moja wa kumbi kubwa nchini humo. Mbali na hivyo, pia kuna kumbi binafsi za mikutano midogo midogo kwa ujumla wake zinaweza kupokea watu 10,000.

Mahusiano mazuri ya nchi mbili hizo yazaa matunda

Mnamo Februari 2022, Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, alitembelea DRC kama sehemu ya kukuza uhusiano kati ya Uturuki na nchi hiyo.

Wakati wa ziara yake, rais Erdogan alitia saini mikataba kadhaa kuhusu usalama, ulinzi na miundombinu na nchi hiyo. Moja ya mikataba hii ilihusisha kampuni ya Kituruki ya Milvest, ambayo DRC iliifadhili awali dola milioni 290 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Kifedha cha Kinshasa.

Kulingana na vifungu vya mkataba vilivyokubaliwa kati ya DRC na Uturuki, miundombinu yote yenye ubora wa juu itakayojengwa na Milvest itakuwa mali ya DRC baada ya miaka 49 ya uongozi wa kampuni hiyo.

Mwenyekiti wa kampuni ya Milvest Turhan Mildon ameiambia TRT Afrika kuwa wakati wanatekeleza ujenzi wa mradi huu moja ya changamoto kubwa walizokutana nazo ilikuwa ni usafirishaji wa vifaa kutoka Uturuki hadi DRC.

‘‘Tulifanya uchunguzi mapema tulijipanga vyema, na kuna vifaa ambavyo tulivihitaji badala ya kuvisafirisha kutoka Uturuki bali tuliwekeza katika viwanda hapa na tukazalisha hapa hapa DRC,’’ anasema Mildon.

Watu Zaidi ya 1500 walihudhuria hafla ya ufunguzi huku Wakongo wakijawa na furaha nyusoni mwao wakionesha kufurahishwa na uzinduzi wa kituo hicho.

Mbali na raia wa wakongo, wakiwemo Waturuki na wafanyabiashara wa kigeni waishio nchini DRC walifika kwenye ufunguzi huo.



 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG