USAMBAZAJI WA MABANGO YA ELIMU TAHADHARI YA MAGONJWA YA MLIPUKO WAENDELEA HANANG
Na. Elimu ya Afya kwa Umma.
Katika kujiweka tayari katika kukabiliana na Magonjwa ya Mlipuko hususan katika maeneo yaliyoathiriwa na Mvua ikiwemo Hanang, usambazaji wa mabango ya uelimishaji umeendelea katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kituo cha Afya Katesh Wilayani Hanang Mkoani Manyara.
Miongoni mwa jumbe zilizomo katika mabango hayo ni pamoja na mbinu za kujikinga na Magonjwa ya Kuhara na Kutapika ambazo ni kunywa maji yaliyochemshwa au kutibiwa na dawa ya Klorini, kutumia choo kwa usahihi kila wakati na kutupa kinyesi cha mtoto katika tundu la choo na pia kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni baada ya kutoka chooni, kabla ya kula au kumlisha mtoto na baada ya kugusa maji ya mafuriko au tope.