WASAMBAZAJI WA PEMBEJEO ZA KILIMO WALALAMA UPUNGUFU WA MBEGU SOKONI, SERIKALI YAWATAKA KUUNGANA NA KUFANYA KAZI KWA PAMOJA.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Tehama Wizara ya Kilimo Rashid Likiligo, Akiongea jambo na waandishi wa habari kwenye mkutano huoPeter Kazungu Mratibu wa Farm to Market alliance, akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari
Natisile Mollel ambaye ni muuzaji wa pembejeo Wilayani Kiteto Mkoani Manyara,
Sehemu ya washiriki wa mkutano huo
NA JOHN BANDA, DODMA
KATIKA msimu wa Mvua za Masika
zinazoendelea Kunyesha Nchini kote zimeleta Neema kwa Mkulima anaelima na
kutarajia mavuno, lakini pia kwa wasambaza Pembejeo ambao kipindi hiki ndiyo
hasa kipindi cha kuchuma fedha kutokana na wateja wa nyenzo hizo kuongezeka.
Pia Wakulima huhitaji kupata
pembejeo ili kufanya shughuli zao lakini zimebainika baadhi ya changamoto
ambazo huenda zikaleta ugumu kwa wakulima, na moja wapo Ikiwa ni kupanda kwa
gharama ya pembejeo kama v ile mbegu sokoni.
Changamoto hizo zimethibitishwa
DESEMBA 15,2023 jijini,Dodoma na Natisile Mollel ambaye ni muuzaji wa pembejeo
Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, alipoongea na
waandishi wa mbalimbali vyombo vya habari wakati wa mkutano wa wadau wa
pembejeo za Kilimo ulioandaliwa na Farm to Market Alliance.
“uhitaji wa mbegu sokoni hasa
kipindi hiki cha masika ambapo katika maeneo Mengi ya nchi mvua zinaendelea
kunyesha, huku upungufua ukiwa ni mkubwa na kusababisha bei kupanda,
Naweza nikasema kuwa hata bei za
mbegu zimeongezeka kwani tofauti na mwaka jana ambapo jumla tuliuza 1500 kwa
kilo mbili lakini kipindi hiki tunauza 1800 kwa kipimo hichocho”, amesema
Kwa Upande wake Kaimu Mkuu wa Kitengo cha
Tehama Wizara ya Kilimo Rashid Likiligo
amewaasa wasambazaji wa pembejeo hapa nchini kufanya kazi na serikali
ambayo ndiyo yenye watu, nguvu na sauti hasa kipindi hiki ambacho huduma ya
kilimo inatolewa kwa M - KILIMO
Naye Peter Kazungu Mratibu wa
Farm to Market alliance amesema mradi huo ambao una lengo la kuwafikia kila wakiulima
wote kwa kuwarahisishia wasambazaji kufanya kazi zao kwa urahisi Kigijitali, ambapo
kwa Tanzania Mradi huo unafanya Kazi kwa takribani Mikoa sita.