Mwenyekiti wa Chana cha ACT Wazalendo Mkoa wa Dodoma, Yohana Mussa akifafanua jambo wakati akitoa Tamko la Kuyakataa maandamano yaliyotangazwa na CHADEMA , Kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari jijini Dodoma leo .
Mwenyekiti wa Chama cha ADC Mkoa wa Dodoma, Lailath Mbuta akisistiza Jambo kwenye Mkutno huo na Waandishi wa Habari
...........................................
NA JOHN BANDA,
DODOMA
WATANZANIA
wameshauriwa kulipuuza Tangazo la Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe la kuwataka
Kushiriki maandamano Aliyotangaza kufanyika Januari 24 mwaka huu kwa lengo la kuishinikiza
Serikali kuzingatia maoni na mapendekezo ya wadau wa uchaguzi nchini.
Hivi karibuni chama
cha CHADEMA kupitia mwenyekiti wake Ffreeman Mbowe kilitangaza maandamano ya Amani
Bila kikomo Nchi Nzima, hadi Pale Serikali Itakapofanyia kazi Maoni na
Mapendekezo ya Wadau kuhusu upatikanaji wa Katiba Mpya na Chaguzi huru na Haki,
ambapo alisema maandamano hayo yanatarajiwa kuanza siku ya Jumatano ya Tarehe
24 mwezi huu.
Alisema Maoni ya wadau
hao yalitolewa wakati Muswada wa sheria
ya uchaguzi wa Rais, Wabunge, na Madiwani wa mwaka 2023, Muswada wa sheria ya
tume ya taifa ya uchaguzi wa mwaka 2023, na Muswada wa Sheria ya malekebisho ya
sheria ya vyama vya Siasa ya mwaka 2023, ilipotolewa maoni Bungeni jijini
Dodoma hivi karibuni.
Viongozi hao wa Baadhi
ya vyama vya Siasa Mkoani Dodoma wameyasema hayo mbele ya waandishi wa Vyombo
mbalimbali vya habari jijini humo, ambapo wamewataka wananchi na wanachama wote
vyama vyao kuyapuuza maandamano hayo na kuendelea na kazi zao za ujenzi wa
taifa kwa kuwa mchakato bado unaendelea Bungeni.
Akiongea kwenye
mkutano huo Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Mkoa wa Dodoma Yohana Mussa amesema, Maandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliyoyaita ya Amani
Ukweli ni kwamba hayana Baraka na Ndani yake hayatakuwa ya Amani.
"Sisi kama Chama
cha ACT Wazalendo na wenyeviti wenzangu tunaamini maoni yetu yatazingatiwa na
wabunge kwa kuwa tumeiona nia njema ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na Serikali
yake Katika jambo hili, " Amesema.
"Kwanini Sisi Wenyeviti tusema Maandamano
haya sio ya Amani?, ni kwa Kuwa CHADEMA kimeacha mchakato halali wa majadiliano na
fulsa iliyotolewa na Rais,Samia ya Maridhiano Kisiasa na kujenga umoja wa
kitaifa lakini cha kushangaza, MBOWE na watu wake wanataka kuwaingiza watu
barabarani kufanya maandamano katika nyakati hizi ambazo taifa letu linahitaji
utulivu mkubwa, " Amesema Mwenyekiti huyo
Naye Mwenyekiti wa
Chama cha wananchi (CUF) Stephen Chitema amewaka wabunge kuzingatia maoni
yaliyotolewa kikao cha Bungeni, kuhusu mabadiliko ya katiba kwani Jambo hilo ni la muda mrefu na limekuwa likitumia
fedha nyingi.
Kuhusu maandamano ya
tarehe 24, amesema Freeman Mbowe ameitisha maandamano ya wafuasi wake na
wananchi, wakati ambao wananchi wapo mashambani wakiendelea na kilimo,
"Kwa wito huu
anataka wananchi watoke kwenye shughuri za kilimo waje mijini kuandamana hii
sio sahihi, " Amesema
Amesema Mbowe
anaitisha maandamano katika jiji la kibiashara Dsm huku akitambua juhudi
zilizofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan kufungua frusa za uwekezaji na
biashara katika jiji ilo.
"Lengo hapa sio
maandamano ya Amani ila ni uharibifu wa juhudi za Mhe. Rais Katika Kuifungua
Nchi
"Sisi Wenyeviti
wa Vyama Vya Upinzani Tuliopo Makao Makuu ya Nchini Tunampongeza Rais DK. Samia
Suluhu Hassan Kwa Uamuzi Wake wa Kupeleka Bungeni Marekebisho ya sheria ya
uchaguzi ambapo sasa, kamati ya kudumu ya bunge ya katiba na sheria chini ya
mwenyekiti wake Joseph Mhagama imetoa fulsa kwa wadau mbalimbali kutoa maoni
yao Hivyo CHADEMA wajue kila mtu atatoa maoni kwa wakati wake,
Amesema kamati ya
bunge ilitoa ushirikiano wa kutosha kwa wadau KIASI cha kutosha ilifikia baadhi
ya wadau walipewa nafasi Zaidi ya mara moja kutoa maoni yao wakiwamo hawa
wanaitisha maandamano
"Chama cha
Chadema na Mwenyekiti wao Freeman Mbowe imekuwa ni tabia yao kuacha
michakato halali na kukimbilia kwa wananchi kujilizaliza, Sisi wenyeviti Imara
tunasema hatuungi mkono maandamano hayo na tunalaani kwa nguvu kubwa ukiukaji
huu wa maridhiano ya kidemokrasia yalianzishwa na Rais Samia Suluhu Hassan,
" Amesema

Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Mkoa wa Dodoma, Stephen Chitema akizungumza katika mkutano huo na Waandishi wa Habari

Mwenyekiti wa Chama cha AAFP Davis Sembuche Mkoa wa Dodoma, akichangia jambo katika mkutano huo.

Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi Meshack Masinga akiongea jambo katika mkutano huo

Mwenyekiti wa Chama cha Democrasia Makini Mkoa wa Dodoma, Baraka Machumu akizungumza jambo kwenye Mkuno huo.


Waandishi wa habari wakiufuatilia mkutano huo wa baadhi ya viongozi wa Vyama vya Siasi, uliofanyika jijini Dodoma leo Januari 18,2024