BANDA MEDIA BLOG

Pakistan yashambulia Iran siku mbili baada ya shambulio la kombora

 

Pakistan imesema kuwa imefanya mashambulizi ya makombora katika nchi jirani ya Iran, siku mbili baada ya shambulio la Iran kuzidisha uhasama kati ya mataifa hayo ya nyuklia.

Pakistan ilisema mashambulizi hayo yamepiga "maficho ya kigaidi" katika eneo la mpakani la Sistan-o-Balochistan.

Vyombo vya habari vya Iran vimeripoti kuwa wanawake watatu na watoto wanne wameuawa.

Wawili hao wamekuwa wakilaumiana kwa muda mrefu kwa kuhifadhi makundi ya wapiganaji wanaofanya mashambulizi katika maeneo ya mpakani mwao.

Siku ya Jumatano jioni, vyombo vya habari vya Iran viliripoti kwamba milipuko kadhaa ilisikika karibu na mpaka na Pakistan, karibu na mji wa Saravan.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Pakistan ilithibitisha mashambulizi hayo katika taarifa yake, na kusema kuwa "idadi isiyojulikana ya magaidi waliuawa wakati wa operesheni hiyo ya Kijasusi".

Hatua hiyo ya kijeshi ya Pakistan inajiri baada ya kulaani vikali shambulio la Iran siku ya Jumanne, ambayo ilisema iliua watoto wawili.

Iran ilisema mashambulizi yake yalilenga kundi la waasi lenye makao yake Pakistan, lakini Pakistan ilisema raia waliuawa.

Ilikuwa imeionya Tehran juu ya "madhara makubwa" kwa hatua hiyo "haramu" na ikapiga marufuku balozi wa Iran kurejea nchini na pia ilimuondoa mjumbe wake kutoka Pakistan.

Iran ilisisitiza kuwa mashambulizi yake yalilenga tu Jaish al-Adl, ambayo inalitaja kuwa kundi la kigaidi, na sio raia wa Pakistan.

Hata hivyo jirani yake wa mashariki alikasirishwa na hatua hiyo.Pakistan ilisema imetokea "licha ya kuwepo kwa njia kadhaa za mawasiliano".

Siku ya Alhamisi, Pakistan ilitetea mashambulizi yake yenyewe katika ardhi ya Iran, ikisema hatua zake zililenga tu "magaidi" wanaojulikana kama Sarmachars.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG