Januari 18, 2024
Na Mwandishi Wetu Zanzibar
Hatua ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kuitaja Tanzania miongoni mwa mataifa 10 ya Afrika yenye deni dogo la taifa imedhihirisha mafanikio ya mageuzi ya kiuchumi yanayoendelea nchini tangu Rais Samia Suluhu Hassan aingie madarakani karibu miaka mitatu iliyopita.
Chini ya utawala wake, Rais Samia ameongeza maradufu uwekezaji wa serikali kwenye miundombinu na huduma za jamii, ikiwemo sekta za elimu, maji, afya, umeme na kilimo.
Uwekezaji wa serikali, hususan kwenye ujenzi wa miundombinu, umechochea ukuaji
wa uchumi nchini.
Kupitia mkakati wa Royal Tour, Rais Samia pia ameongeza kwa kiasi kikubwa sana
idadi ya watalii wanaokuja nchini.
Ongezeko la watalii limeleta pesa za kigeni nchini na kuongeza ajira.
Vilevile, Serikali yake imeongeza bajeti kwenye sekta ya kilimo kwa kiwango ambacho hakijawahi kuonekana tangu nchi ipate uhuru na hivyo kuongeza tija kwa wakulima nchini.
Sera rafiki za Serikali ya Samia kwa sekta binafsi zimesaidia kuongeza kasi na ukubwa wa uwekezaji wa makampuni ya nje na ya ndani.
Mikopo nafuu yenye riba ndogo na muda mrefu wa marejesho imepunguza mzigo wa
deni la taifa.
Pamoja na kwamba Tanzania imeendelea kukopa nje ili kuwekeza kwenye miradi ya maendeleo, ukopaji makini wa Serikali ya Rais Samia wa kutumia mikopo nafuu badala ya mikopo yenye masharti ya kibiashara na ukuaji wa kasi kubwa wa Pato la Taifa (GDP), vimepunguza mzigo wa deni la taifa.
Takwimu za kimataifa zinaonesha kuwa jumla ya deni duniani sasa hivi ni Dola za Marekani trilioni 307, ambayo ni sawa na asilimia 336 ya GDP ya dunia.
🇨🇩 DRC 11.1%
🇧🇼 Botswana 18.1%
🇪🇹 Ethiopia 31.2%
🇬🇼 Guinea Bissau 31.5%
🇬🇶 Equatorial Guinea 33.7%
🇰🇲 Comoros 36.9%
🇹🇩 Chad 38.7%
🇨🇲 Cameroon 39.6%
🇳🇬 Nigeria 41.3%
🇹🇿 Tanzania 41.8%
Nchi 10 duniani zenye kiwango
kikubwa cha deni (uwiano wa Deni la Taifa kulinganisha na GDP) hizi hapa:
Japan🇯🇵 264%
Singapore 🇸🇬 160%
Italia 🇮🇹 145%
Marekani 🇺🇸 129%
Hispania 🇪🇸 113%
Canada 🇨🇦 113%
Ufaransa 🇫🇷 112%
Uingereza 🇬🇧 101%
India 🇮🇳 89%
Argentina 🇦🇷 85%
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania imevitaka vyama
ambavyo havijachaguza viongozi wake kufanya hivyo, kabla muda kuisha.
Hii ni kufuatia ofisi hiyo kubaini uwepo wa idadi kubwa wa vyama vya siasa ambavyo muda wa viongozi wake kukaa madarakani umefikia kikomo, kufikia mwaka huu.
"Kwa mujibu wa sheria, kila chama cha siasa kinapaswa kufanya uchaguzi wa kidemokrasia wa viongozi wake kwa vipindi ambavyo vimewekwa katika Katiba yake...vilevile uchaguzi wa viongozi wa chama cha siasa unapaswa kufanyika sio zaidi ya miaka mitano tangu uchaguzi uliopita kufanyika," inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.
Tanzania ina jumla ya vyama vya siasa 19, vyenye usajili kamili kutoka ofisi hiyo.
