BANDA MEDIA BLOG

YPDEA YAMUOMBA RAIS KUWATENGENEZEA WANAWAKE NA VIJANA MADHINGIRA RAFIKI...!!!

 YPDEA imemuomba Rais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan  na Serikali yake kutengeneza Mazingira  rafiki ya Kujiajili ikiwemo kwenye Kilimo ili kuwaepusha  baadhi ya wanawake kujihusisha na Biashara za ngono wanazoangukia baada ya kukata tamaa kimaisha.


Mshauri wa Rais wa Taasisi ya YPDEA Vicent Malendaa Akifafanua jambo wakati alipokuwa akizungumza na viongozi wa taasisi hiyo mkoa wa Dodoma.

Wajumbe wa Taasisi ya Kiraia ya YPDEA mkoani Dodoma wakiwa katika kikao chao kilichofanyika jijini Humo.

    Msahuri wa Rais wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya YPSEA Vicent Malendaa, Afisa Kilimo Taifa Neema Chiboni, Mratibu Idara ya Vijana na wanafunzi wa Vyuo vikuu na Sekondari Ashura Moshi, Mwenyekiti wa Mkoa wa Dodoma Frank Tesha na viongozi wa Halmashauri za wilaya na manispaa wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kikao hicho.                           

                                       …………………………………………

                                          NA JOHN BANDA, DODOMA

 TAASISI ya Kiraia ya YPDEA imemuomba Rais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan  na Serikali yake kutengeneza Mazingira  rafiki ya Kujiajili ikiwemo kwenye Kilimo ili kuwaepusha  baadhi ya wanawake kujihusisha na Biashara za ngono wanazoangukia baada ya kukata tamaa kimaisha.

 Pia kuisadia Serikali kwa kuhamasisha amani kuanzia ngazi za mitaa, kata, mikoa hadi Taifa kwa kufichua Waovu na maovu yaliyopo katika jamii

 Mratibu wa Vijana na Wanafunzi wa vyuo Vikuu na sekondari wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya YPDEA inayojishughulisha na Vijana kwenye Maswala ya Amani, Uchumi na Maendeleo, Ashura Moshi alipoongea na waandishi wa habari kando ya kikao cha taasisi hiyo Kimkoa kilichofanyika jijini Dodoma.

 “Tunamuomba Rais Samia na Serikali yake waweke mazingira wezeshi kwa wanawake yatakayowawezesha kujiajili katika miradi mbalimbali ikiwemo kuwatengea maeneo ya kilimo kwa kuwa kila mmoja atakapojibidiisha kwa kazi,

 Watu wakifanya kazi zao katika mazingira ya kuvutia watajenga uchumi wao na hatimaye vitendo hatarishi kama vya biashara hatarishi za ngono kwa baadhi ya wanawake, Madawa ya Kulevya na vitendo vya ushoga kwa baadhi ya vijana wenzetu vitapungua kama siyo kwisha kabisa”, amesema

 Awali Mshauri wa Rais wa Taasisi hiyo Vicent Malendaa, akiongea kwenye Kikao hicho amesema moja ya Majukumu ya Taasisi hiyo ni pamoja na Kuwakusanya vijana pamoja na kuwatia moyo wa kuendelea na maisha kwa kujishuhulisha bila kukata tama, huku YPDEA ikiwatafutia na kuwanganisha na fursa mbalimbali za kiuchumi.

 Aidha amesema katika moja ya Tafiti zake alizowahi kufanya aligundua kuwa sababu kubwa ya kufanya familia nyingi kuwa katika Mdororo wa Kiuchumi, pamoja na kukosa maendeleo ni kutoaka na Baadhi ya wanandoa kuishi bila amani kunakosababishwa na kiburi cha Fedha na kazi kwa Mwanamke Huku Mwanaume akikataa kuonewa, hivyo taasisi hiyo itahakikisha inatoa Elimu ya Umuhimu wa Amani kwa ngazi zote.

 Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mkoa wa Dodoma, Frank Tesha amesema Vijana wengi wanapofeli kwenye mipango yao ya kimaisha kupitia shughuli wanazokuwa wakifanya, wanajikuta wametumbukia  katika mambo ya uvunjifu wa maadili unaopelekea wengi wao kupoteza Dira nzima ya maisha ambapo YPDEA ipo kwa ajili ya kuwashika mkono na kuwarejesha tena katika matumaini mapya.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG