Polisi wa Uturuki wamekamata watu 47 wanaoshukiwa
kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la Daesh katika miji mikubwa, ikiwemo mji
mkuu wa Ankara, na Istanbul, amesema Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki Ali
Yerlikaya kupitia mtandao wa X.
Operesheni Bozdogan-6 imefanywa kwa pamoja siku ya
Jumatano Adana na Bursa, ikiratibiwa na Kurugenzi ya Usalama wa Taifa na
Kitengo cha Kupambana na Ugaidi.
Miongoni mwa waliokamatwa waliohusishwa na Daesh,
watu 22 walikamatwa Istanbul, 1 Kirikkale, 15 Ankara, 2 Adana, na 7 Bursa.
Akihimiza dhamira ya amani ya taifa na umoja,
Yerlikaya amesema, "Kwa amani, umoja, na mshikamano wa nchi yetu pendwa,
hatutawapa nafasi yeyote katika magaidi hao."
'Vita vyetu vitaendelea'
Ameonyesha umuhimu wa jitihada za vikosi vya ulinzi,
akisema, "Tutaendelea na mapambano yetu bila kusitishwa kwa jitihada za
vikosi vyetu vya ulinzi."
Imefanya jumla ya opereshini 1,162 dhidi ya Daesh
tangu Juni 1, 2023, polisi wa Uturuki wamewakamata washukiwa 2,402, waziri
amesema.
Uturuki imekuwa nchi ya kwanza kuitaja Daesh kama
shirika la kigaidi, imekumbana na mashambulizi kadhaa kutoka kwa kundi hilo.
Zaidi ya waathirika 300 wamepoteza maisha yao, na
mamia zaidi wamejeruhiwa katika mauaji 10 ya mabomu ya kujitoa mhanga, na
mashambulizi manne ya silaha.
