Waziri Mkuu wa Uingereza Rishi Sunak ameweka hatma yake ya baadaye ya kisiasa katika kuona kupitishwa mpango huo - uliowekwa kwa mara ya kwanza na Waziri Mkuu wa wakati huo Boris Johnson mnamo Aprili 2022 - kuwafukuza mara moja wahamiaji wanaofika kwenye ufuo wa Uingereza kwenda Rwanda / Picha: AP
Waziri Mkuu wa Uingereza Rishi Sunak
alipata mshtuko mwingine Jumatatu wakati Bunge la Malodi lilipitisha
marekebisho matano kuhusu mswada wake mpya wa Rwanda.
Marekebisho hayo, yakiidhinishwa,
yatafanya iwe vigumu kwa Baraza la Commons kutangaza Rwanda kuwa nchi
"salama" na itaitaka serikali kuzingatia sheria za ndani na
kimataifa.
Iwapo itapitishwa kuwa sheria,
marekebisho hayo yangeathiri pakubwa lengo kuu la mswada huo mpya kwani
mabadiliko yanayohitajika yatarahisisha majaji kuupinga.
Katika hali mbaya sana, hata hivyo,
Baraza la Malodi lilipiga kura ya kuchelewesha mkataba wa kati wa Sunak na
Rwanda wa uhamiaji katika kile kilichoripotiwa kuwa ni mara ya kwanza kupiga
kura dhidi ya kuidhinishwa kwa mkataba huo kwa zaidi ya muongo mmoja.
Kamati ya pande zote ilisema ulinzi
katika mkataba huo "haujakamilika" na lazima utekelezwe kabla ya
kuidhinishwa.
Mpango wa kuwapeleka Rwanda wanaotafuta hifadhi nchini Uingereza umezua pingamizi kutoka kwa watetezi wa haki za biandamu / Picha : Reuters
Mswada huo unalenga kushughulikia maswala ya Mahakama ya Juu ya Uingereza, ambayo iliamua kwamba mpango wa awali wa serikali wa kutuma waomba hifadhi nchini Rwanda ulikuwa kinyume cha sheria.
Mswada huo unawalazimu majaji kuchukulia
Rwanda kama nchi salama na unawapa mawaziri mamlaka ya kupuuza sehemu za Sheria
ya Haki za Kibinadamu.
Mpango wa Rwanda umekuwa mojawapo ya
mipango yenye utata zaidi ya sera ya serikali ya uhamiaji kwani ilizua ukosoaji
wa kimataifa na maandamano makubwa kote Uingereza.
Mnamo Januari mwaka jana, Sunak alisema kuwa kukabiliana na vivuko vya boti ndogo na wahamiaji wasio wa kawaida katika Idhaa ya Kiingereza ilikuwa kati ya vipaumbele vitano vya serikali yake kwani zaidi ya wahamiaji 45,000 waliwasili Uingereza kwa njia hiyo mnamo 2022.

