BANDA MEDIA BLOG

SHEKH MKOA WA DODOMA ATAKA WAUMINI KUOMBEA MSHIKAMANO KWENYE UCHAGUZI

 

NA JOHN BANDA, DODOMA

KUELEKEA uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Mwezi Octoba mwaka huu na Ule Mkuu utakaofanyika Mwakani Waumini wa Dini ya Kiislam wametakiwa kuiombea Serikali Inayoongozwa na Dk. Samia Suluhu Hassani iweze Kunyooka  

Wito huo Umetolewa leo June 17,2024 na Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Alhaji Mustafa  Shaban wakati alipokuwa akitoa Mawaidha kwa Waumini Hao waliokuwa kwenye Ibada ya Eid Ul Adha iliyofanyika katika msikiti wa Gadafi.

Shekhe amesema wakati nchi inajiandaa kuelekea kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Mwezi wa 10 mwaka huu na ule wa Mwakani nivizuri kila Muumini Kuiombea Nchi na Serikali yake.

“kila muumini ajiombee yeye mwenyewe, Familia yake, Jamaa inayomzunguka, Nchi na Serikali inayoongozwa na Dk. Samia Suluhu Hassan  ili kila kitu kikiwa kimenyooka vizuri  uchaguzi huo utakuwa wa amani na salama”, amesema

Aidha amesema waendelee kuombea Upendo, Mshikamano, Ushiriano na Umoja wa Kitaifa.

Akiongelea Eid Ul Adha amesema ni siku za Mfungo zinazofungwa kwa siku kumi hasa kwa namba Shufaa zinazoanzia 2,4,6, 8 siku ya 10 ndiyo shufa yenyewe na zote zinazogawanyika ambapo pia ni suna kufunga tarehe 9.

 







Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG