Msanii huyu wa Muziki wa Bongofleva Joseph Francis maarufu kwa Mandojo amefariki dunia leo August 11, 2024, akipatiwa matatibu mkoani Dodoma.
Msanii mwenzake aliyefanya naye kazi kwa ukaribu Domokaya na Soggdogghunter wamethibitisha taarifa hiyo ya kifo cha Mandojo.
Kwa mujibu wa taarifa za awali Mandojo amefariki kwa kupigwa na wananchi waliodhani kuwa ni mwizi baada ya kutokea mtafaruku kati yake na mtu mmoja ambaye alimuitia mwizi....!!!!
