BANDA MEDIA BLOG

VODACOM NA AFYACHECK WAMUENZI BABA WA TAIFA KWA KUTOA HUDUMA ZA AFYA

 

..........................................

NA JON BANDA,DODOMA

KAMPUNI ya Mtandao wa simu ya Vodacom Tanzania LTD kwa kushirikiana na Taasisi ya AfyaCheck wanamuezi Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kutoa huduma za Afya Bure katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma huku wakiwa na malengo ya kuwahudumia watu Elfu tano katika mikoa mitano.

Mratibu wa Kambi za Afya za twende Butiama Africa, Dkt. Isack Maro leo Oct 5,2024 amewaambia waandishi wa Habari jijini humo kuwa,  wanachokifanya kwenye Kambi hizo ni Pamoja na Kuwapima wagonjwa, Kuwapa dawa, Ushauri na Elimu ambapo huduma zote ni bure.

 Amesema kambi hizo za kupima Afya zilizodhaminiwa na Vodacom Foundation Tanzania, zinalenga kumuenzi Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kuwapima na kuwatibu wanaosumbuliwa na Shinikizo la Juu la Damu, Kisukari, Saratani ya Kizazi na matiti kwa wanawake na Tezi Dume kwa wanaume ikiwa ni Pamoja na kuwahudumia Watoto na watu wazima.

Aidha amesema huduma hizo zimeanza kutolewa tangu jana oct 4 watamaliza jumapili oct 6 mwaka huu, kisha watatoa huduma kama hizo katika mikoa ya Singida, Tabora, wilaya ya Bihalamuro Kagera na Chato mkoani Mwanza.

Mkazi wa Chang’ombe jijini Dodoma, Mzee Husein Ninga ameipongeza AfyaCheck kwa kuja na mpango huo wa kutoa huduma za Afya hasa kwa wazee wenye umri mkubwa kwani kwa kufanya hivyo ni kumuenzi Hayati Baba wa Taifa kwa Vitendo.

Hayati Baba wa Taifa la Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alifariki Tarehe 14,10,1999 ambapo watanzania wataungana kote Duniani kwenye kumbukizi ya miaka 25,  oct 14,mwaka huu.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG