NA JON BANDA,DODOMA
ILI wakazi wa Halmashari ya jiji la Dodoma waweze
kuepukana na magonjwa ya Mlipuko yakiwemo matumbo ya kuhara yanayosababishwa na
uchafu, Watendaji wa Kata na Mitaa wametakiwa kutoa elimu kwa wananchi namna ya
kutunza mazingira ikiwemo kutumia sheria ya adhabu kwa wachafuzi wa makusudi.
Afisa Mazingira na Udhibiti wa Taka Ngumu wa Jiji la
Dodoma Ally Mfinanga amejitokeza mbele ya Waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari
na kuwataka wahusika kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi
“nitoe maelekezo kwa watendaji wa kata, mitaa, maafisa
afya na mazingira waliyopo kwenye kata na mitaa kuhakikisha wanatoka maofisini
kwenda kutoa elimu kwa vitendo, mwananchi akiwa ameelimika nab ado akaendelea
kuchafua mazingira apewe adhabu kama sheria za mazingira zinavyoelekeza”,
amesema
Aidha Mfinanga ameongeza kuwa halmashari hiyo imeyaagiza
makapuni ya uzoaji taka na kuzipeka Chidaya kuimarisha magari yao na kuwa na
vifaa vya kutosha kwa ajili ya kazi hiyo hasa kipindi hiki cha kuelekea msimu
wa mvua.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Wafanyabiashara
Soko la Sabasaba, Kombo Kombo amesema kumekuwa na ucheleweshaji mkubwa wa kuzoa
takataka zinazozalishwa kwa wingi kwenye dampo lililopo sokoni hapo
“niseme bila kupepesa macho Pamoja na mtu tuliyepewa
na jiji, kwa ajili ya kusimamia usafi sokoni, bado changamoto inakuwa kwenye
usombaji wa taka ambazo zimekuwa zikibaki hata kwa zaidi ya wiki nzima kutokana
na kukosekana kwa magari ya kusombea kwa wakati hali inayosababisha wafanyabiashara
kuishi kwa hofu ya maganjwa ya mlipuko”,
Aidha amesema wanaiomba serikali kuondoa takataka kwa
wakati lakini pia watengeneze mitaro ya kupitishia maji machafu.