Askofu wa Kanisa Anglikana Tanzania Dayosisi ya Rift Valley John Lupaa akifafana jambo wakat alipokuwa akiifunga Warsha hiyoiliyowajumuisha washiriki 50 toka wilaya ya Manyoni Mkoani Singida
..................
NA JOHN BANDA, SINGIDA
ASKOFU wa
Kanisa Anglikana Tanzania Dayosisi ya Lift Valley John Lupaa Amefichua Athali
zinazosababishwa na Ubaguzi wa Kimalezi unaofanywa na baadhi ya wazazi na
walezi kwa kuwalundikia kazi wanazozani ni nzito Watoto wasiowazaa wakidhani
wanawakomoa kumbe ndiyo wanawatengeneza, huku wakiwaacha Watoto waliowazaa
wakiwa hawana uwezo wa kujitegemea.
Askofu Lupaa ameifichua siri hiyo wakati alipokuwa Akifunga
Warsha ya pili ya mitaala ya Rasilimali CCMP, iliyoandaliwa na Ushirika wa Wamama
wa Kikristo (UMAKI) wa Kanisa Anglikana Tanzania, ambapo amesema kuwa
kinachowatafuna Watoto wa matajiri mpaka kujikuta hawana uwezo wa kufanya kazi
za kujihudumia ni kudekezwa na wazazi wao.
Amesema siku hizi baadhi ya vijana wa kike na wakiume
wanashindwa kujisimamia katika Maisha yao na wengine kushindwa hata kupika
kufanya usafi wa nyumba, kwa sababu walilelewa kimayaimayai kwa wazazi ama
walezi wao kuwalundikia kazi Watoto baki walioishi nao wakiwemo mabinti wa
kazi.
Ametoa mfano kuwa watu wa nchi za magharibi hasa
wazungu walibweteka wakisema kazi nzito wapewe wenye Ngozi nyeusi, wakati wao
wakijipa kazi za kuwaongoza na kuwasimamia, baadae Weusi walijikuta ndiyo
wabunifu na wavumbuzi wa mwanzo wa mambo ya maendeleo Duniani, Hvyo kumpa mtu
kazi kwa lengo kumkomoa ni kumnoa.
“wazazi/walezi walidhani wanawapenda sana Watoto wao
na kuwanyima kufanya kazi za usafi wao, wa nyumba, kupika wakidhani wanawapenda
sana huku kazi hizo wakiwalundikia mayaya, mabinti wa kazi na Watoto wasiowahusu
bila kujua kuwa ndiyo wanawatengeneza”, amesema
Aidha amesema kuwa hali hiyo imekuwa ni tatizo kwa baadhi ya wanawake ambao wamekuwa wakishindwa kuwapikia chakula hata waume zao
Akiongelea kuhusu mafunzo hayo Askofu Lupaa, amesema ametoa
mwaka mmoja kwa parishi zote za Dayosisi hiyo kuhakikisha zinaweka kitega
uchumi kwenye kila kanisa kwa lengo la kuzitumia Rasilimali na fursa za
kiuchumi ili kujiletea maendeleo.
Nae Afisa
maendeleo wa Dayosisi ya Rift Valley, Kasisi Canon, Ezra Machasa amesema jumla
ya washiriki 50, wameshiriki mafunzo hayo ndani ya siku 6 ambapo wamejifunza
utambuzi wa rasilimali na jinsi ya kuzitumia ikiwemo kuzitambua fursa ambazo
Mungu amewapatia ili kuzitumia kwa ajili ya kujikwamua Kaiuchumi.
“changamoto kubwa iliyopo kwenye jamii ni watu wengi
kutozitambua Fursa wala Rasilimali ambazo Mungu amewapati, hata kama
wanazitambua bado hawazitumii ndiyo maana mradi wa CCMP umekuja ili kuwahamasisha kuzitambua na
kuzichangamkia ili wajipatie maendeleo ndani ya kanisa”, amesema
Hata hivyo washiriki hao ndiyo watakaokuwa
wawezeshaji waw engine makanisani mwao.
Katibu wa Ushirika wa Wamama wa Kanisa la Anglikana Tanzania (UMAKI) Ley Canon Dkt. Margaret Ndonde akaiongea jambo wakati wakfunga mafunzo hayo
Kwa upande wake Katibu wa Ushirika wa Wamama wa
Kikristo wa Kanisa la Anglikana Tanzania (UMAKI) Lay Canon, Dkt Margaret Ndonde
akiongea kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Kanisa Hilo amesema wamekuja na mradi huo
mahususi wa Mchakato wa kuhamasisha maendeleo ya kanisa na jamii (CCMP) kwa
lengo la kuifumbua macho jamii ya kuziona fursa na Rasilimali zilizopo.
Tunawajengea uwezo ili wao wakawafundishe wenzao
makanisani, ili kanisa lenyewe liwe nuru na chumvi hatimaye liwavute wanajamii,
pia tunatamani mafunzo haya yakawanufaishe wanakanisa kwanza na baadae wayapeleke
katika jamii,
“kanisa liwe nuru na chumvi kwa maana ya mafunzo haya
yawasaidie kwenye maendeleo ya kanisa na jamii.
Aidha amesema Mradi huo unaendelea kwenye Dayosisi 13
za kanisa angalikana hapa nchini huku malengo yakiwa ni kuzifikia Dayosisi zote
28 za kanisa hilo, “tunajivunia pia mradi mwingine wa uundwaji wa vikundi vya
Akiba na mikopo unaotekelezwa kwenye Dayosisi 19 na kwamba tayari asilimia
kubwa ya vikundi vilivyoundwa vimeshasajiliwa kisheria”, amesema