NA JOHN BANDA, DODOMA
KAMISAA wa Sensa Tanzania, Anna Makinda amewambia
wanawake na Samia kuwa Ushindi wa Rais huyo wa Sasa kwenye uchaguzi wa Mwaka
ujao hautaki Maneno Matupu unataka vitendo hasa kujiandikisha na kupiga Kura.
Akiongea kwenye Hafra ya Wanawake na Samia Gala, iliyifanyika
jijini Dodoma ikiwahusisha wanawake hao Kutoka mikoa Nane Nchini Makinda
amesema Ushindi kwenye uchaguzi ujao siyo wa Hiyenahiyena wala perepete za
mdomoni pekee.
Kamisaa Huyo ambaye ni Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amesema ili
Rais Samia Suluhu Hassan aweze kushinda kwa kishindo kwenye uchaguzi ujao
wanawake hao wahakikishe Wanawahamasisha Wananchi wajiandikishe na kisha kwenda kupiga Kura.
"Ni kweli Wanawake mnafanya Kazi nzuri ya
Kumuunga Mkono Rais Samia kwenye Kazi anazofanya kwa ajili ya watanzania, ila
kumbukeni Ushindi kwenye uchaguzi ujao si wapelepete mdomoni Tu au kuimba
hiyena hiyena unataka vitendo, msibaki kuimba mkasahau kuhamasishana kupiga
Kura zitakazompitisha mama 2025", amesema
Aidha Makinda amesema Rais Samia ni Rais tuliyopewa na
Mungu kwani wakati akiapishwa wengi walimbeza lakini sote ni mashahidi kwa
Kazi kubwa alizofanya mpaka sasa, Kwa
ajili ya Jamii ya Watanzania, hata wanaume wenyewe wanashangaa amewezaje.
Kwa upande wake Mbunge wa Dodoma mjini Anthon Peter Mavunde, amewapongeza wanawake na Samaia kwa Kazi Nzuri wanayoifanya ambapo aliwaunga mkono kwa kuwaahidi kuwanunulia Vyombo na kuwaongezea mtaji kwa ajili ya kuanzisha mradi wa Mapishi
Naye mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amelielezea
kundi hilo la wanawake na Samia kuwa limejipambanua nchi nzima kwa ajili ya
kumuunga mkono na kumtia Moyo Rais Samia kwa vitendo
Amesema Miaka ya hivi karibuni wanawake walikuwa
wanagombea nafasi za uongozi kwa uoga na mashaka kutokana na kutojiamini,
lakini sasa wamepewa ujasiri na Rais aliye madarakani kwa uongozi wake mahili
na wa kuigwa tena akiwa mwanamke.
Awali akisoma Risala mwenyekiti wa Wanawake na Samia
mkoa wa Dodoma, Fatuma Mdidi amesema Kazi
ambazo wameshazifanya ni Pamoja na kuibua vitendo vya ukatili 47, walivyofanyiwa
wanawake na Watoto, kuukijanisha mkoa kwa kutengeneza vyungu vya maua, ushiriki
wa mbio za mwenge, kutoa elimu ya maadili, misaada mbalimbali kwa makundi
yasiyojiweza Pamoja na kushiriki shughuli za kiserikali ikiwemo kuhamasisha
jamii kujiandisha kwenye Daftari la mpiga kura mwaka huu.
Ameongeza kuwa walioshiriki katika hafla hiyo ni pamoja
na wanawake kutoka mikoa 8, ya Tanzanzia Bara na kwamba kwenye uchaguzi ujao wa
mwaka 2025 wanasimama na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wa CCM.