Tundu amemng'oa madarakani Freeman Mbowe ambaye amekiongoza chama hicho kwa miongo miwili.
Mbowe amekuwa wa kwanza, kukiri kushindwa na kumpongeza Lissu kupitia mtandao wa X.
Lissu naye ametumia mtandao wa X kutangaza ushindi wake.
Matokeo rasmi ya uchaguzi huo uliofanyika jana usiku bado hayajatangazwa.
Hii ni taarifa ya hivi punde, tutaendelea kukujuza kadri tunavyopokea taarifa.
Tags
SIASA
