Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwan Jakaya Kikwete amewataka Maaafisa Kazi Wafawidhi nchini kuongeza ubinifu katika usuluhishi wa migogoro mahala pa kazi wito alioutoa Morogoro wakati alipofungua kikao kazi 12 Septemba 2025.
Na. OWM-KVAU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi,
Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete amewaagiza Maafisa Kazi
Wafawidhi nchini kuendeleza ubunifu katika utendaji wao wa kazi huku wakizingatia
maadili ya utumishi wa umma.
Amewasisitiza kutoa huduma bora na kwa wakati
hususani katika maeneo nyeti yanayohusisha usuluhishi wa migogoro ya kikazi na
malalamiko ya wananchi mara yanapofikishwa kwenye ofisi zao.
Maafisa Kazi Wafawidhi toka mikoa ya Tanzania Bara wakiwa kwenye kikao kazi cha kuandaa mwongozo wa ukaguzi mahali pa kazi mjini Morogoro 12 Septemba 2025.
Waziri Ridhiwani alieleza hayo Septemba 12,
2025 mkoani Morogoro wakati wa Kikao kazi cha kuandaa mwongozo wa ukaguzi
mahali pa kazi ili kujumuisha masuala ya wafanyakazi wa Nyumbani, Watu wenye
Ulemavu na Utumikishwaji wa Mtoto.
Katika hatua nyingine, amewataka Maafisa hao
kuongeza juhudi za kutoa elimu kwa jamii kwa kushirikiana na wadau wa Utatu
amba oni Serikali, vyama vya waajili ana vyama vya wafanyakazi katika
kushughulikia changamoto za kikazi.
Kikao hicho kiliwahusisha viongozi wa Idara ya Kazi, Msajili wa Vyama Vyama vya Wafanyakazi, pamoja na Maafisa Kazi Wafawidhi wa Mikoa yote Tanzania.


