Katibu wa Wanawake na Samia Mkoani Dodoma, Neema Ndashao akiwalisha Keki wanafunzi wa Shule ya Msingi Kaloleni jijini humo, wakati wa hafla ya kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwake.
Katibu wa Wanawake na Samia Mkoani Dodoma, Neema Ndashao akipanda mti katika Shule ya Msingi Kaloleni jijini humo, wakati wa hafla ya kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwake.
NA JOHN ISRAEL, BANDA MEDIA DODOMA
WANAWAKE na Samia Mkoa wa Dodoma Januari 27,2026 wameungana na wanafunzi wa
shule ya msingi kaloleni jijini humo Pamoja na watanzania kwa ujumla kumtakia Heri ya
Kuzaliwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyezaliwa mnamo mwaka 1960. Kwa
kupanda miti ya matunda Pamoja na kukata keki ya Upendo
Akiongea katika hafla hiyo iliyofanyika katika shule
ya msingi Kaloleni jijini humo Katibu wa Wanawake hao Mkoa wa Dodoma, Neema
Ndashao amesema wamepanda miche ya miti 30 ya matunda kwa lengo la kumuunga
mkono Rais Samia kwa kutimiza miaka 66
Ndashao amesema, Rais Samia ndiye kinara wa mazira
hapa nchini tangu akiwa makamu wa Rais, na kwamba amekuwa akisisitiza umuhimu wa
kupanda miti na kutunza mazingira.
“tunamuunga mkono mama Samia kwa kupanda miti ili
kulinda na kutunza mazingira, Pamoja na kukata keki ya upendo na wanafunzi
tukisherekea pamoja naye siku yake ya kuzaliwa”, amesema
Nae Mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Kaloleni,
Jackison Jumbe ambapo Tukio hilo limefanyika amesema shule hiyo imetenga eneo
la bustani ya matunda maalumu, na kwamba wataitunza miti hiyo ili itakapoonza
kuzaa matunda yawafae wanafunzi
“tunashukuru kitendo cha wanawake na samia kuja
kupanda miti shuleni kwetu, inasaidia kutunza mazingira ukizingatia rais
katujengea majengo mapya, hivyo matunda yakianza yatawasaidia wanafunzi kupata
mlo kamili”, amesema
kwa upande wake mwalimu Selina Nyagawa anayefundisha
darasa la tatu akisimamia Idara ya Mazingira shuleni hapo, amesema kila mti
utakabidhiwa mwanafunzi wa kuutunza hivyo hakuna utakaokufa ikizingatiwa kuna
maji ya kutosha shuleni hapo
“tunampongeza Rais Samia kwa Siku yake ya Kuzaliwa,
tutaitunza hii miti mpaka izae Matunda kwa ajili ya nafunzi, pia tumuahidi
kufanya kazi kwa weredi na kuwapa Watoto matokeo tarajiwa”, amesema
wanafunzi
wamemshukuru Rais Samia na kumtakia Maisha marefu, huku wakimpongeza kwa
kuihudumia shule hiyo kwa kuijengea miundombinu Pamoja na vyumba vya madarasa.
Ikumbukwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan Amitimiza jumla ya Miaka 66 tangu kuzaliwa kwake.