
Licha ya changamoto hizo, “Le Professeur” hakuacha kuipongeza Morocco kwa ukomavu wa kimichezo na uandaaji wa kiwango cha juu ulioshuhudiwa katika michuano hiyo ya 35 ya Kombe la Mataifa ya Afrika. Wenger alipongeza nidhamu na moyo wa ushindani (sportsmanship) ulioonyeshwa na Morocco muda wote wa mashindano, akitaja kuwa shirika na miundombinu ilikuwa ya “ajabu na isiyoaminika.” Sifa hizi kutoka kwa Wenger zinazidi kuimarisha hadhi ya Morocco kama taifa linaloweza kuandaa matukio makubwa ya soka ulimwenguni, ikiwa ni maandalizi ya kuelekea Kombe la Dunia 2030.
Kauli hii ya Wenger inakuja wakati ambapo mchezo huo wa fainali dhidi ya Senegal ulitawaliwa na hisia kali na migogoro ya uwanjani, hali iliyopelekea Rais wa FIFA, Gianni Infantino, na kocha wa Morocco, Walid Regragui, kulaani vurugu zilizotokea. Hata hivyo, tathmini ya Wenger inatoa mtazamo tofauti kwa kuthamini ubora wa soka na uwezo wa Morocco kuhimili dhoruba za kisaikolojia. Kwa Wenger, AFCON 2025 imekuwa kielelezo cha ukuaaji wa soka la Afrika, hasa kwa kuona makocha wazalendo wakiongoza timu zote nne zilizofika nusu fainali.