GEITA; MAKAMU wa Rais wa Tanzania Dk Emmanuel Nchimbi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka mitano ya kifo cha Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli.
-Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela alitoa taarifa hiyo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari na kueleza maadhimisho hayo yatafanyika Machi 17, 2026, wilayani Chato.
-Shigela alisema Dk NchimbI anatarajiwa kuwasili mkoani Geita leo mchana kupitia uwanja wa ndege wa Chato.
-Alisema misa na maadhimisho hayo yatahudhuriwa pia na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi ambaye atawasili mkoani Geita kesho.
-Alitaja viongozi wengine wanaotarajiwa kuhudhuria shughuli ya maadhimisho hayo ni Makamu wa Rais Mstaafu, Dk Philip Mpango na Waziri Mkuu mstaafu, Kassim Majaliwa.
-Alisema tukio hilo limeratibiwa na familia ya Dk Magufuli kwa kushirikiana na serikali, ambapo litatanguliwa na misa takatifu.
-Alisema misa hiyo ya kumuombea na kumuenzi itafanyika nyumbani kwake Chato na kuongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge Ngara, Severine Niwemugizi.
- Alisema maadhimisho yataanza rasmi leo kwa matukio mbalimbali ya kijamii ikiwa ni pamoja na mbio zitakazoanza asubuhi kuelekea Hospitali ya Wilaya ya Chato.