BANDA MEDIA BLOG

MIUJIZA YAMWAGIKA KWENYE KONGAMANO LA WANAWAKE KAGERA

 

Askofu wa Kanisa Anglikana Tanzania Dayosisi ya Kagera Darlington Bandankeha akifurahia jambo wakati alipokua akizungumza kwenye kongamano hilo 



                                                  .......................................

Mratibu wa Utume na Uinjilisti Kanda ya ziwa wa Kanisa la Angilikana Tanzania Rev Happyness Ndunguru Chanai amewapongeza wanawake zaidi elfu 25 waliokutanika kwenye kongamano la Maombi Duniani lililofanyika Mkoani Kagera.

Amesema Kongamano hilo limezaa matunda ya Wokovu kwa wanawake 700 huku wengine wakipokea miujiza ya uponyaji na baraka za Mungu, huku akiwataka wanawake hao kutunza wokovu pamoja na miujiza waliipokea kwa kuendelea kumtafuta Mungu kwa njia ya maombi na kujifunza zaidi neno la Mungu..

Mratibu wa Utume na Uinjilisti Kanda ya ziwa wa Kanisa la Angilikana Tanzania Rev Happyness Ndunguru Chanai

“kupata wokovu, miujiza ni jambo moja ili kuvitunza lazima udumu katika maombi na kujifunza neno la Mungu kwa bidi ili uendelee kukua kiroho”, amesema

Kongamano hilo ambalo hufanyika kila mwaka ki Dunia mwezi kama huu, limewakutanisha wanawake wa kanisa hilo kanda ya ziwa katika Dayosisi ya Kagera chini ya  Askofu Darlington Bandankeha huku likiongozwa na neno kutoka kitabu cha Mathayo 11:28 Njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha.

“hakika Mungu ametupumzisha, amefanya mambo makubwa kwa wanawake wa kanda ya ziwa, jina la Bwana libarikiwa"

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG