BANDA MEDIA BLOG

SHIRIKA LA STAMICO LAFUTARISHA RAMADHAN NA KWARESMA WATU WASIOJIWEZA ZAIDI 400

 







         NA JOHN ISREAL, DODOMA

MKURUGENZI wa Shirika la Taifa la Madini (STAMICO), Dkt. Venancy Mwase amesema kitendo cha Waumini kukutana katika Mfungo wa Ramadhan na Kwaresma ni funzo toka kwa Mungu linalomaanisha Watanzania wote ni wamoja.

Dkt. Mwase ametoa kauli hiyo kwenye tukio la kuwafutarisha makundi mbalimbali wakiwemo Wajane, Wagane, Watoto wanaoishi bila huduma za wazazi, watu wenye ulemavu na Washirika wenza wa Biasahara ya Nishati saafi,  wakiwemo wanawake na Samia mkoa wa Dodoma

“tangu nimekuwa sijawahi kuona watu wa dini hizi kubwa kufunga kwa wakati mmoja, watanzania ni wamoja, Tanzania siyo nchi ya udini, Mungu ametupa funzo ndiyo maana leo tumekaa tunakula pamoja,

hii mimi siiti Futari naita chakula cha Upendo, watu wa makundi mbalimbali wamekutana wamekaa na kula pamoja huu ni upendo ulioje unaojengwa na shirika lenu la stamico na niwaambie tu Futari hii itaendelea kila mwaka”, amesema

aidha amesema shirika hilo linalohudumia wachimbaji wadogo wa madini hapa nchini litaendelea kuyawezesha makundi mbalimbali katika uchumi shirikishi ikiwa ni pamoja na mpango wa kuwawezesha Watoto wenye mahitaji maalum…

 Mgeni Rasmi katika hafla hiyo, Katibu Tawala msaidizi anayeshughulikia Uwekezaji, viwanda na Biashara mkoa wa Dodoma Mwajabu Nyamkomori, amelipongeza shirika la STAMICO ambalo limewawezesha wachimbaji wadogo wa madini kupiga hatua za kimaendeleo.

Aidha pongezi na shukurani nyingine zimetoka kwa mwenyekiti wa Wanawake na Samia Fatuma Madidi, pamoja na Mkurugenzi wa Foundation for Disabilities Hope ambao ni washirika wenza katika Biashara ya Nishati safi kwa kushirikiana na STAMICO.

Walioshiriki katika Futari hiyo ya Ramadhan na Kwaresma ni pamoja na makundi ya watoto Yatima kutoka ntyuka, Kisasa na Miyuji,Watu  Walemavu wa ngozi chini FDH (Foundation for Disabilities Hope), walemavu wa viungo kutoka kituo cha Samaria Hombolo, chini ya Shivyawata, wajana, wagane, pamoja na wanachi wa kawaida

 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG