BANDA MEDIA BLOG

JESHI LA POLISI MKOA WA DODOMA LIMEJIPANGA KUIMALISHA ULINZI KATIKA KIPINDI CHOTE CHA SIKUKU ZA MWISHO WA MWAKA

 Vikosi vya ulinzi shirikishi vikipokea maelekezo ya namna ya kukabiliana na uhalifu katika kipindi hiki cha sikuku za mwisho wa mwaka.

Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma David Misime akitoa maelekezo namna ya kukabiliana na uhalifu kipindi cha sikuku za Chrismas na Mwaka mpya nje ya jengo la polisi  mkoa

Magari ya polisi yatakayotumika katika ulinzi


Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma tumejipanga kikamilifu katika kuhakikisha Maadhimisho ya sikukuu katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka 2015 na mwanzo wa mwaka 2016. Siku kuu zinazotarajiwa kusherehekewa ni MAULID itakayofanyika katika Misikiti mbalimbali tarehe 24/12/2015 itakayofuatiwa na Mkesha wa X- Mass katika Makanisa mbalimbali hadi siku yenyewe ya X- Mass tarehe 25/12/2015 na hatimaye tarehe 01/01/2016 Sikukuu ya mwaka mpya.

Tutaimarisha ulinzi katika maeneo mbalimbali ya biashara na mikusanyiko ya watu. Tutafanya kazi hiyo kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola ili kuhakikisha yeyote mwenye nia ovu ya kufanya uhalifu wa aina yeyote anadhibitiwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Kamati za ulinzi na usalama katika nyumba za ibada na makampuni ya ulinzi binafsi nao washiriki kikamilifu ili kuhakikisha ulinzi unaimarika na ibada zinafanyika bila bughudha ya aina yeyote.

Wanacnhi wote wakazi wa Dodoma na wageni watakao kuwa hapa Dodoma katika kipindi hiki cha siku kuu za mwisho na mwanzo wa mwaka kuchukua tahadhari za kiusalama, washerehekee kwa amani na utulivu  na shamra shamra zao zisivunje sheria.

Wazazi wahahikikishe watoto wao hawaendi katika kumbi za starehe na bar bali wanasherehekea katika mazingira salama wakiwa chini ya uangalizi makini, ulinzi majumbani uimarishwe wasiache nyumba peke yake. Wamiliki wa kumbi za starehe wahakikishe hawajazi watu kupita kiasi, wahakikishe usalama ni wa kutosha katika kumbi zao.

Aidha watumiaji wote wa barabara wazingatie sheria za usalama barabarani na hasa waendesha vyombo vya moto wazingatie udereva wa kujihami na kuhakikisha kwenye makazi ya watu hawaendeshi vyombo vya moto zaidi ya spidi 50kph kama sheria za usalama barabarani kifungu cha 51 kinavyoelekeza. Kuepukana na ulevi kupita kiasi na kutoendesha magari wakiwa wamelewa ili kuepusha ajali zisizozalazima.

Kila mmoja ni vizuri akatambua kuwa usalama unaanza na yeye mwenyewe na maana halisi ya sikukuu hizi ni kumtukuza Mungu na kudumisha amani na pale watakapotilia shaka jambo lolote watoe taarifa Polisi ili kupatiwa msaada wa haraka. Ninawatakia sikukuu njema zenye amani na utulivu.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG