BANDA MEDIA BLOG

RAMIRES KAKAMILISHA USAJILI WA KUIHAMA CHELSEA

Ramires 1
Kiungo wa Chelsea Ramires amekamisha usajili wake wa kujiunga na klabu ya China Jiangsu Suning kwa ada ya uhamisho inayoaminika kufikia £25m.
Mbrazil huyo mwenye miaka 28 amekubali mkataba mpya wa miaka minne lakini alipata nafasi ya kuanza kwenye mechi saba pekee za Premier League msimu huu.
Jiangsu iliyomaliza ikiwa nafasi ya tisa kwenye msimu wa mwaka 2015 inanolewa na beki wa zamani wa The Blues Dan Petrescu.

Ramires aliisaidia Chelsea kushinda mataji ya Premier League, FA Cup, League Cup, Champions League pamoja na Europa League.
Akiwa Chelsea Ramires alicheza mechi 251 akafanikiwa kufunga mabao 34 tangu ajiunge na klabu hiyo akitokea Benfica kwa kitita cha pauni milioni 17 hiyo ilikuwa ni mwaka 2010

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG