Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
akipokewa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman leo jijini
Dar es salaam wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini. Rais,
Dkt. John Magufuli alikua mgeni rasmi.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
(katikati) akisalimiana na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria
leo jijini Dar es salaam.
Wimbo
wa Taifa ukipigwa wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Sheria. Kulia ni
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (Kulia) akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman
Baadhi
ya Viongozi waliohudhuria Maadhimisho ya Siku ya Sheria wakiwa
wamesimama wakati wimbo wa Taifa ukipigwa. Kutoka kulia ni Jaji Mkuu wa
Kenya Dkt. Willy Mutunga, Jaji Kiongozi wa Tanzania Mhe. Shaaban Lila
(katikati) na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Said Mecki Sadiki.
Baadhi
ya Viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini na wadau muhimu wa
Mahakama waliohudhuria Maadhimisho ya Siku ya Sheria wakitoa heshima zao
wakati wimbo wa Taifa ukipigwa.
Rais
wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Charles Rwechungura akitoa
salam na ujumbe wa Chama hicho wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria
leo jijini Dar es salaam.
Katibu
Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (kulia) akifuatilia hotuba
zilizokuwa zikitolewa na viongozi mbalimbali wakati wa maadhimisho ya
Siku ya Sheria. Kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama Bw. Hussein
Katanga.
Jaji
Mkuu wa Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman akiwahutubia
viongozi, mabalozi na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi
waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Sheria.
Tags
HABARI KITAIFA







