![]() |
| Moja ya Kaburi lililopo katika Mashamba hayo yenye Mgogoro katika ya wakazi wa Mapinduzi na Mwenzao kijini hapo, Kaburi hilo lilizikwa mwak 1958 |
![]() |
| Baadhi ya wakulima wa Kijiji cha Mapinduzi wakiwa wamekusanyika katika Eneo la Mgogoro ambalo walikuwa wakilitumia kwa kilimo. |
![]() |
| Joyce Fundi miaka 982) mwenye Jembe akieleza jambo kuhusu Makaburi hayo na Jinsi shamba lake pamoja na ya wakulima wengine yalihatalini kutaifishwa. IMETENGENEZWA NA BANDA BLOG |
Na Lydia Kishia,
Dodoma
ZAIDI ya Wakulima 60 wa Kijiji cha Mapinduzi ‘A’ kata ya Nghong’onha manispaa ya Dodoma wanawasiwasi wa
kunyang’anywa mashamba yao yenye ukubwa wa Hekari 237 kutokana na mkazi mwenzao
aliye na nia ya kuwadhulumu kwa vitisho vya kutumia polisi ikiwemo kuburuzwa
mahakamani huku wakikosa msaada wowote toka kwa viongozi wa ngazi za juu.
![]() |
| Wakulima hao wakiwa mashambani |
Walimesema kuwa mkazi huyo anayejulikana kwa jina la Mchiwa
Chedego ambaye anataka kuwadhulumu eneo lao amekuwa akiwaleta wawekezaji na
kuwaonyesha eneo hilo bila hata ya kuujulisha uongozi wa kijiji hicho
Pia wamewaomba viongozi wanaohusika na masuala ya Ardhi
kufika katika kijiji hicho na kuchunguza eneo hilo kwani haiwezekani eneo lote
la kijiji hicho likawa la mtu mmoja na wakati hata wazazi wake walikuwa hawana
eneo kubwa kama hilo
Wananchi hao wamesema kuwa Chedego amekuwa akifungua kesi
mara kwa mara mahakamani kwa lengo la kutaka kuchukua eneo hilo kwa nguvu kutokana
na yeye kuwapa fedha polisi na huku wao
kushindwa kesi kwa kuwa ni maskini na hawana fedha za kuwapa polisi hao
Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho Willy Joseph amemuomba mkuu wa
mkoa na mkuu wa wilaya kuingilia kati
mgogoro huo na kuweza kuutatua kwani ndilo eneo ambalo wakulima hao wanajipatia
kipato cha kukidhi mahitaji yao muhimu

Nae Diwani wa Kata ya Nghon’oha Philip Namga alisema kuwa
Mgogoro huo ameukuta ni wa Muda mrefu sasa lakini hawezi kuuzungumzia kwa kuwa
shauri hilo lipo mahakama ya Wilaya lakini kwa sasa anamsubiri Mbunge wa Jimbo
la Dodoma Mjini Anthon Mavunde ambaye kwa sasa Yupo jijini Dar es Laam kwa shuhuli
za kiserikali ili afikishie Taarifa hiyo ili ajue jinsi ya kuwasaidia wapiga
kura wake.
Bado juhudi za kumapata Chedego ili aweze kutoa ufafanuazi
wa Tuhuma dhidi yake zinaendelea kutokana na kutokuwepo kijijini hapo wakati
waandishi walipofanya ziara kijijini hapo.

Tags
HABARI KITAIFA







