BANDA MEDIA BLOG

POLISI DODOMA YAKAMATA MAGOBOLE 7 HUKU MENGINE 19 YAKISALIMISHWA NA WAMILIKI WAKE



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA



TAARIFA YA KAMANDA WA POLISI MKOA WA DODOMA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE 11.03.2016

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma limefanya Operesheni na Msako mkali katika Wilaya zake zote na kukamata makosa mbalimbali. Operesheni hiyo ilianza kufanyika tarehe 22/02/2016 hadi 06/03/2016.

Katika Operesheni hiyo jumla ya silaha haramu 19 aina ya Gobore zimesalimishwa na silaha saba (7) zimekamatwa za watu waliokaidi utii wa sheria, mitambo miwili ya kutengeneze silaha hizo haramu imekamatwa pamoja na watuhumiwa saba ambao ni:-


Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma Lazoro Mambosasa akionyesha Magobole hayo kwa waandishi wa habari PICHA ZOTE NA BANDA BLOG

1.   KHAMISI MTANDIKA, mwenye miaka 40, mkuliama alikamatwa akiwa na silaha moja aina ya gobore, mideki mtatu ya kusafishia silaha, baruti gramu 12 na goroli.
2.   MAJUTO MAGANA, mwenye miaka 31, mkulima alikamatwa na gobore moja.
3.   JAVAN WILLIAM, mwenye miaka 36, mkulima alikamatwa na gobore moja.
4.   COSMAS MASWAGA, mwenye miaka 55, mkuliama alikamatwa na gobore moja na mtambo mmoja wa kutengenezea silaha.
5.   MBARAKA KITINDI, mwenye miaka 45, mkulima alikamatwa na gobore moja na mtambo mmoja wa kutengenezea silaha.
6.   COSMAS EZEKIEL MKENZA, mwenye miaka 34, mkulima alikamatwa na gobore moja.
7.   SANYA MZOGOLE, mwenye miaka 45, mkulima alikamatwa na gobore moja.
 
Watuhumiwa wote ni wakazi wa kijiji cha MANDA Tarafa ya MPWAYUNGU Wilaya ya Chamwino Mkoa wa Dodoma  na wamekuwa wakimiliki silaha hizo kinyume cha sheria  na wakizitumia katika uhalifu mbalimbali hasa uwindaji haramu katika hifadhi ya RUAHA inayopakana na mkoa wa Iringa. Kutokana na operesheni hiyo watu 19 waliweza kusalimisha silaha zao katika ofisi za serikali za vijiji na hawakuchukuliwa hatua kwa kuwa walitii sheria bila shuruti.

Katika Wilaya za Dodoma, Kondoa na Kongwa walikamatwa watuhumiwa 32 wa makosa ya Kupatikana na Bhangi, jumla ya misokoto misokoto 672 ilikamatwa.  Watuhumiwa 11 walikamatwa kwa kosa la Kupatina na Pombe haramu ya Moshi na jumla ya lita 260 zilikamatwa.  Watuhumiwa 7 walikamatwa kwa kosa la Kupatikana na madawa ya kulevya aina ya Mirungi Kilogram 43.
 
Pia Operesheni ilihusisha makosa ya Usalama barabarani na kukamatwa kwa jumla ya pikipiki 265 kwa makosa mbalimbali, ambapo pikipiki 241 zilitozwa faini na kiasi cha fedha Tsh. 7,230,000/= zilipatikana kutokana na tozo. 
Napenda kutoa wito kuwa, Msako mkali unaendelea na watu wote wanaomiliki silaha haramu kinyume cha Sheria wasalimishe silaha hizo kwa hiari kwenye  Ofisi za Serikali na vituo vya Polisi mapema iwezekanavyo na hawatachukuliwa hatua.  Wale wote wanaomiliki silaha kinyume cha Sheria wasiotayari kusalimisha wafichuliwe ili wachukuliwe hatua za kisheria dhidi ya umiliki haramu wa silaha. Aidha wananchi waache kujihusisha na vitendo vya uhalifu wa aina yoyote na kufanya kazi halali kujipatia kipato halali kwa familia zao kwani msako utakuwa endelevu wasije wakaishia jela na kuziacha familia zao zikiteseka.


Imetolea na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi wa Polisi  (ACP- LAZARO BENEDICT MAMBOSASA.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG