BANDA MEDIA BLOG

RAIS MAGUFULI AWASILI MWANZA, AAMURU BARABARA UWANJA WA KAYENZE IFUNGULIWE MARA MOJA


1
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akishuka kwenye ndege mara baada kwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Mwanza wakati alipopitaka mkoani humo akielekea Nyumbani kwake Chato mkoani Geita kwa ajili ya mapumziko, hii ni mara ya kwanza kwenda kupumzika kijijini kwake toka alipchaguliwa na kauapishwa kushika madaraka ya kuongoza Jamhuri ya Muungano ya Tanzania mwezi Oktoba mwaka jana.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela amemshukuru Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli mara baada ya kuamuru kufunguliwa kwa barabara inayopita kandokando ya uwanja wa ndege kuelekea Kayenze iliyokuwa imefungwa kwa miezi miwili na kuleta adha kubwa kwa wananchi wanaoishi maeneo hayo.
Mara baada ya Rais Magufuli kuamuru barabara hiyo ifunguliwe mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani Mwanza  Uongozi mzima wa mkoa huo waliongozana kwenda Kayenze na kuwatangazia wananchi kwamba wako huru kutumia barabara hiyo kwakuwa Mh. Rais ameamuru ifunguliwa na sisi tumekuja kutekeleza agizo la rais na sasa barabara hii imefunguliwa. 
(PICHA NA JOHN BUKUKU- FULLSHANGWE-MWANZA)
2
Mke wa Rais Mama Janet Magufuli akishuka kwenye ndege wakati Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli alipowasili uwanjani hapo akielekea Chato Mkoani Geita kwa mapumziko.
3
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa mwanza leo.
4
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mh. Baraka Konisaga kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza leo.

5
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza.
6
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na viongozi wa kamati ya Amani mkoani Mwanza wakati alipowasili uwanjani hapo akielekea Chato.
7
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mh.Altaf  Mansour  mlezi wa shirikisho la Vyuo vikuu CCM  Kanda ya Ziwa, Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela.
9
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mh.Altaf  Mansour  mlezi wa shirikisho la Vyuo vikuu CCM  Kanda ya Ziwa, Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela.
10
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana wana  CCM  waliofika uwanjani hapo kumpokea, Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela.
11
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akipigiwa saluti na mmoja wa wakuu wa vyombo vya ulinzi na  usalama mkoani Mwanza waliofika uwanjani hapo kumpokea.
12
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana afisa habari wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza Bw. Atley Kuni .
13
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akielekea kukagua vikundi vya ngoma na kwaya.
14
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli na Mkewe mama Janet Magufuli wakiangalia vikundi vya ngoma wakati walipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Mwanza leo wakielekea Chato kwa mapumziko.
15
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli  na Mkewe Mama Janet Magufuli wakiwapungia wachenza goma wakati wa mapokezi kwenye uwanja wa Ndege wa Mwanza.
16
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na askari wa kikozi cha Zimamoto uwanjani hapo.
17
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiangalia kwaya ya AIC Makongoro ambayo iliimba wimbo wa kuhamasisha kuitunza amani ya nchi na kumhamasisha kiasi cha kumfanya kujumuika nao na kuimba pamoja na wanakwaya hao.
18
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiimba pamoja na wanakwaya wa AIC Makongoro ya jijini Mwanza wakati wa mapokezi kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza.
19
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiimba pamoja na wanakwaya wa AIC Makongoro ya jijini Mwanza wakati wa mapokezi kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza.
20
Wadau Issa Michuzi kulia na Pius Lugonzibwa kushoto walikuwepo katika mapokezi hayo.
21
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akwapungia mkono wafanyakazi wa uwanja wa ndege wa Mwanza.
22
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na baadhi ya wananchi waliofika kumpokea kwenye uwanja wa ndege wa mwanza katikati ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela  na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mh. Baraka Konisaga.
23
25
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela akimshukuru Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli mara baada ya kuamuru kufunguliwa kwa barabara inayopitka kandokando ya uwanja wa ndege kuelekea Kayenze.
26
Mh.Altaf  Mansour  mlezi wa shirikisho la Vyuo vikuu CCM  Kanda ya Ziwa alikuwepo katika mapokezi hayo , Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mh. Baraka Konisaga.
27
Baadhi ya wanahabari waliokuwepo uwanjani hapo wakifurahia kwa kugonganisha chupa za soda kinywaji ambacho Mh. Rais Dk John Pombe Magufuli alitoa ofa kwa wananchi wote waliokuwepo uwanjani hapo, kulia ni Shila Kutoka ITV Mwanza na kushoto ni Atley Kuti afisa habari wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza.
28
Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli akiondoka kwenye kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza mara baada kupata kifungua kinywa kwenye mgahawa wa Victoria Catering.
29
Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli akipiga picha ya pamoja na kwaya ya AIC Makongoro na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Mwanza kabla ya kuelekea Chato mkoani Geita.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG