——————–
CHAMA
cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimewataka wananchi wanaoishi katika
maeneo yanayomilikiwa na chama hicho kuhakikisha wanafunga mikataba
rasmi ili kuepuka usumbufu wakati maeneo hayo yatakapohitajika kwa
ajili ya shughuli za kichama.
Kimesema
kuna baadhi ya wananchi waliopewa maeneo ya kuishi kwa muda kwa nia ya
kuwasaidia na badala yake wameyageuza kuwa makaazi yao ya kudumu jambo
ambalo sio sahihi.
Akizungumza
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Ndg. Vuai Ali Vuai kwa nyakati
tofauti katika mwendelezo wa ziara ya kuhakiki mali na maeneo mbali
mbali yanayomilikiwa na CCM huko Mbweni Mkoa wa Magharibi Kichama.
Alisema
chama kinaendelea na zoezi la kuhakiki mali zake kutokana na kuongezeka
kwa vitendo vya udanganyifu vinavyofanywa na baadhi ya watu wasiokuwa
waaminifu wanaotengeneza hati na mikataba bandia ya kujimilikisha mali
za chama hicho kinyume na utaratibu.
Ndg.
Vuai alifafanua kwamba katika hatua za kupunguza kero hizo chama
kimeamua watu wote ambao wamepewa kibinadamu sehemu za kuishi ama
kufanya biashara kwa muda katika maeneo yanayomilikiwa na CCM wafunge
mikataba rasmi ili chama kiweze kunufaika na rasilimali zake.
“
Watu waliopewa kwa dharura sehemu za kuishi na kufanya biashara kama
hatujawapa mikataba rasmi inayotambulikana kisheria, ambayo ni
kielelezo cha kumtambulisha nani mmiliki halali wa maeneo hayo baadae
inaweza kuwa fursa ya kufanya utapele na kusababisha usumbufu na lawama
kwa chama.
Tags
SIASA