Toka ukiwa mdogo mpaka unazeeka umekuwa ukijiuliza kwanini kila kitu
unachokula au kukionja huwa kinakuwa na ladha mbaya mara tu baada ya
kusafisha kinywa chako kwa kutumia mswaki ulioweka dawa ya meno.
Dawa nyingi za mswaki huwa zinakemikali zifuatazo Sodium lauryl sulfate,
sodium laureth sulfate (SLS) and sodium lauryl ether sulfate (SLES)
ambazo hupunguza nguvu ya ukinzani ili kutengeneza povu (foaming action)
kwenye dawa ya meno ili kusaidia katika kuondoa mabaki ya vyakula
kwenye kinywa chako.
Lakini pia kemikali hizi hukinzana na utendaji kazi wa taste buds
(huhusika na utambuzi wa ladha) kwa kuvunja vunja phospholipids kwenye
ulimi wako. Matokeo yake husababisha ladha ya uchachu (bitter tastes)
nahii ndo sababu kila unachokionja na kukila huonekana kibaya mara baada
ya kusafisha meno yako.
Lakini hali hii huondoka mara tu baada ya mda mfupi. Niwatoe hofu
watumiaji wa dawa za meno kuwa hali hii ya kuhisi uchachu haina madhara
yeyote kiafya.
Your Health, Our Concern
Tags
AFYA
