BANDA MEDIA BLOG

MAN CITY YA GUARDIOLA YATUPWA NJE NA MONACO LIGI YA MABINGWA ULAYA


 BN
Kikosi cha Vinara wa Ligi Kuu ya Ufaransa timu ya Monaco imeitoa nje klabu ya Man City kwa jumla ya magoli 3-1 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa na kutinga hatua ya robo Fainali.
 
Ushindi wa Monaco unafanya mabao kuwa sare ya 6-6, lakini mabao ya ugenini yanaibeba Monaco ambayo ilifungwa 5-3 jijini Manchester katika mechi ya kwanza.
 
Monaco walipata mabao mawili ya haraka katika kipindi cha kwanza kupitia Mbappe Lottin na Fabinho, yakadumu hadi mapumziko.
Kipindi cha Leroy Sane aliamsha matumaini ya Man City kwa kufunga bao katika dakika ya 71 katika dakika ya 77, Tiomoue Bakayoko akayazima kwa kufunga bao la tatu kwa Monaco ambayo imesonga mbele na kumuacha Kocha Pep Guardiola wa Man City na majonzi rundo.
 
 
VIKOSI
Monaco: Subasic, Sidibe, Raggi, Jemerson, Mendy, Fabinho, Bakayoko, Lemar, Bernardo Silva, Germain, Mbappe-Lottin.
Subs: De Sanctis, Jorge, Dirar, Joao Moutinho, Irvin Cardona, Irvin Cardona, Diallo, Toure.
 
 
Man City: Caballero, Sagna, Stones, Clichy, Kolarov, Sane, Fernandinho, Silva, De Bruyne, Aguero, Sterling.
Subs: Bravo, Zabaleta, Jesus Navas, Delph, Otamendi, Toure, Iheanacho.
 
Referee: Gianluca Rocchi (Italy)

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG