![]() |
| Wafanyakazi wa shirika hilo wakichimba mashimo tayari kwa kupanda miti katika shule ya msingi Mtumba |
![]() |
| Wanafunzi wa shule hiyo wakiwa na Michi ya miti ya vimvuli na matunda kabla ya zoezi la upandaji kuanza |
![]() |
| Wanafunzi wakiendelea na uchimbaji wa mashimo |
![]() |
| Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo KATIBU tawara msaidizi Aziza Mumba akiweka mbolea katika mti aliupanda shuleni hapo |
![]() |
| PICHA YA PAMOJA NA VIONGOZI WA MKOA WA DODOMA WALIOSIMAMA NYUMA |
John Banda, Dodoma
SHIRIKA la Tanzania Girl Guides Association limezindua mradi wa upandaji miti katika shule ya msingi ya Mtumba manispaa ya Dodoma huku likiwa na lengo la kuifanya nchi kuwa ya kijani ili kuweza kuepukana na mabadiliko ya tabia nchi.
Akiongea katika uzinduzi huo Kamishna Mkuu wa Girl Guides nchini Simphorosa Hangi alisema wanakamilisha uzinduzi huo wa kitaifa huku tayari shirika hilo likiwa limeshanza upandaji wa miti hiyo katika mkoa mingine ya Arusha, Lindi na Mwanza
Hangi alisema kuwa kwa sasa wapo katika mikoa 22 na wanaendelea kufanya juhudi ili waweze kukamailisha mikoa yote ikiwemo Zanzibar ambapo kila mkoa watapanda miti 600 huku wakiacha kila mkoa kuendelea na zoezi hilo ili kulifanya Taifa kuwa la kijani.
Nae Mwenyekiti wa Shirika hilo kitaifa Martha Qorro Alisema zoezi hilo linafanyika mashuleni na kuachwa kwa viongozi wa Girl Gaides wa mkoa husika ambao watahakikisha wanapeleka na kupanda miti katika shule ambazo maji yapo yakutosha ili kuifanya miti hiyo kukua
Kwa upande wake Mgeni Rasmi Katibu Tawara msaidizi Aziza Mumba katika uzinduzi huo alisema juhudi hizo zinazofanywa na Shirika la Girl Guides zinafaaa kuigwa ili kusaidia kurejesha uoto wa kijani ambao utasaidia kuyaweka mazingira kuwa mazuri yenye lutuba ya kutosha kutokana na mvua zitakazokuwa zikinyesha kila mahali
Tags
MAZINGIRA





















