BANDA MEDIA BLOG

WABUNGE WA BUNGE LA AFRICA MASHARIKI NA KATI AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA DODOMA ILI KUJUA CHANGAMOTO ZINAZOWAKWAZA KIASI CHA KUTOVUKA MIPAKA

Charles Makongoro Nyerere akiuelezea moja ya mkataba wa Jumuiya ya africa mashariki na kati kwa wafanyabiashara wa Dodoma
Mwenyekiti Charles Makongoro Nyerere katikati akimkabidhi mwenyekiti wa mstaafu wa TCCIA kanda ya Dodoma Faustine Mwakalinga kulia Bendera ya Jumuiya ya africa mashariki na kati mara baada ya majadiriano yao kuhusu changamoto za kibiashara

Kiongozi wa Mkutano wa watanzania waliyopo katika Bunge la Africa mashariki na kati Charles Makongoro Nyerere akizungumza jambo wakati wabunge hao walipokukutana na wafanyabiashara wa mjini Dodma ili kujua changamoto za kibiashara zinazowakwamisha wasivuke mipaka ya jumuiya hiyo
Mwenyekiti wa wabunge wa Tanzania wa Bunge la Africa Mashariki na Kati linalomaliza muda wake june mwaka huu Adamu Kimbisa akifafanua jambo wakati akiongea na wafanyabisahara mjini Dodoma [PICHA NA JOHN BANDA WA BANDA BLOG]


























WAFANYABIASHARA mjini Dodoma wamesema wao siyo waoga kufanya biashara nje ya nchi bali vikwazo vya upatikanaji wa vibali ni tatizo kubwa linalowasababisha  kushindwa kufanya biashara katika nchi wanachama wa Africa mashariki na kati
Wafanyabiashara hao wameitoa kauli hiyo wakati wakiongea na wabunge wa Bunge la Africa masahariki na kati ambao walifika mjini humo kwa lengo la kupata changamoto zinazowakabili kiasi cha kushindwa kufanya biashara zao nje ya mipaka ya Tanzania ambapo kwa upande wake Mtalemwa Mshaju amesema watanzania siyo waoga

Nae Fred Mushi amewaomba wabunge hao kuwasaidia wafanyabiara kuvusha mahindi kutoka nchini Uganda ili waweze kuwauzia Watanzania kwa bei nafuu badara ya kuacha wajanja wachache kuingiza mahindi kwa njia zisizo halali

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wabunge wa jumuiya hiyo nchini Tanzania Adamu Kimbisa akizungumza wakati wa ufunguzi wa mazungumzo hayo yaliyojumuisha wafanyabiashara walio wanachama wa TCCIA amewataka kuchangamkia frusa

Aidha mwenyekiti wa mazungumzo hayo Charles Makongoro Nyerere amesema fursa zipo na wafanyabiashara wanatakiwa kuzichangamkia, huku akiwataka kujiamini kwa kutojiona wanyonge bali waingie katika ushindani kwa ubora wa bidha kama ilivyo kwa mataifa mengine
RIPOTI YA JOHN BANDA, DODOMA

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG