![]() |
| Chuo cha East Africa College kilichofungwa |
| Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Christina Mndeme |
![]() |
| Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo hicho wakiwa ofisini kwa mkuu wa wilaya walikofika kutaka serikali iingilie kati kuhusu malalamiko yao |
MKUU wa Wilaya ya Dodoma mjini Christina Mndeme
amekifunga Chuo cha Uandishi wa habari cha East Africa College huku akimtaka mkuu wa
chuo hicho kuwarejeshea wanafunzi ziadi ya 100 ada zao ndani ya wiki moja
kutokana na kutokuwa na usajili.
Mndeme amelitoa agizo hilo wakati akizungumza na
wanafunzi wa chuo hicho walioandamana mpaka katika ofisi za mkuu wa wilaya
wakitaka usaidizi wa madai yao mbalimbali ikiwemo vyeti vyao baada ya kumaliza
ameutaka uongozi wa chuo hicho kuwarudishia wanafunzi wote wafedha zao za ada na michango mingine katika kipindi cha wiki moja ikiwa ni pamoja kusafisha vyeti vya wahitimu ambao wapo majumbani kwa garama za chuo
Aidha Mkuu huyo wa Wilaya aliwataka wanafunzi
waliosoma na kupata vyeti chuoni hapo kufungua jarada polisi ili hatua za upelelezi
zianze kufanyika na ikibainika kuwa mwenye chuo alikuwa akifanya utaperi kwa kutumia cheti cha mandia atachukuliwa hatua kali ikiwemo ya kufikishwa mahakamni
kwa upande wake Mkuu wa chuo hicho Mshukuru Boeboe amesema amekuwa afuatilia usajili wa chuo hicho tangu mwaka 2012 alipokifungua bila mafanikio lakini akahidi kufanya bidii
"nitafuatilia kwa bidii sana na baada ya muda mfupi nitakifungua chuo changu hivyo wazazi na wanafunzi wasiwe na wasiwasi wowote katika hilo", alisema
Wanafunzi wa chuo hicho Rehema Saimon na Rais wa
wanafunzi Twaha Salim Iddy wakaweka wazi
malalamiko yao ikiwemo fedha nyingi wanazotumia na kumbe chuo hakikuwa na
usajili
"ni wiki mbili sasa tangu kuanza kufuatilia ili tupate haki zetu na sasa tunamshukuru Mungu Dc ametusaidia na tuna imani ya kuzipata fedha zetu ndani ya hiyo wiki moja ili wengine turudi mikoani kwetu ,
tulichanganyikiwa sana baada ya kugungua chuo hakina usajali na kuanza kuwafilia wenzetu ambao tayari walishasoma na kupata vyeti ndiyo maana hawapati mikataba ya kazi hasa waliyopo kwenye maredio bora serikali itusaidie ili baaada e tusije kuutana na tumbua tumbua ya Magufuli", walisema
Chuo hicho kilichopo mailimbili karibu na mnada wa zamani manispaa ya Dodoma kina zaidi ya wanafunzi 100 wa kozi mbalimbali zikiwemo za uandishi wa habari na utangazaji huku wakilipia 800,000, malipo ya mabweni, nauri na chakula
Tags
ELIMU



