![]() |
| Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humfrey Polepole akizungumza nao |

![]() |
| WanaUVCCM waliopo katika shirikisho la vyuo na vyuo vikuu vya mkoani Dodoma wakishangilia jambo kwenye mahafali ya pili ya wahitimu waliyopo katika shirikisho hilo [PICHA NA JOHN BANDA] |
![]() |
| Mnec Anthon Mavunde akizungumza katika mahafali hayo |
![]() |
| Mwenyekiti mstaafu wa Shirikisho la vyuo vikuu Zainab Abdala akizungumza na wanafunzi hao |
![]() |
| Mjumbe Riziwan Kikwete akifurahia jambo wakati akizungumza na wahitimu hao |
![]() |
| Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Martin Shigela akisisitiza jambo katika hafra hiyo |
Na John Banda, Dodoma
Katibu wa Itikadi na uenezi wa Chama cha mapinduzi [CCM]
Humrey Poleple amesema chama hicho kitawafuta uongozi wenyeviti na makatibu wa
mashina na matawi ambao watabainika kupandikiza mabalozi hewa
Polepole ameitoa
kauli hiyo wakati alipokuwa akiongea kwenye mahafali ya pili ya
wanafunzi wa shirikisho la vyuo na vyuo vikuu vya mjini Dodoma ambao ni
wanachama wa CCM
Alisema kumekuwa na migogoro ya mara kwa mara kwa viongozi wa ngazi za Mwenyekiti, Katibu, Mwenezi na Uchumi na Fedha ngazi za wilaya na mikoa hasa kunapokuwa na vyanzo vya mapato katika maeneo yao hali inayowafanya kutoheshimu wanachama.
"inapofika wakati wa uchaguzi viongozi hao kwa kujua kuwa wanachama wanajua maovu yao basi huomua kutafuta kadi na kukodi watu wa maeneo mengine ili waweze kuwapigia kula wao, ninyi muendao huko baada ya kuhitimu mkipata taarifa tuleteeni na ikithibitika tutawafita kazi wahusika wote", alisema
Aidha Polepole amesema katika mageuzi wanayoyafanya
ndani ya CCM mpya ni kuwapandisha mabolozi kuwa na wanachama hai 50 mpaka 150
badala ya nyumba 10 kama ilivyokuwa awali
Awali akizungumza katika mahafali hayo yaliyofanyika
katika ukumbi wa mikutano wa chama hicho wa White House Naibu waziri wa Ajira,
Vijana na Walemavi Anthon Mavunde amesema Wizara imeanziasha Muongozo wa
Uwanajenzi utakaowasaidia wahitimu wa vyuo vikuu kupata mafunzo kwa vitendo
bila vikwazo vya waajili
Tags
polepole














