BANDA MEDIA BLOG

RAIS WA MAURITIUS KUJIUZULU KUTOKANA NA KASHFA YA UFISADI



Rais wa Mauritius kujiuzulu kutokana na kashfa ya ufisadi

Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravind Jugnauth amefichua kuwa rais wa nchi hiyo Ameenah Gurib-Fakim yupo katika ncha ya kujiuzulu kutokana na kashfa ya ufisadi inayomuandama.

Jugnauth aliyasema hayo jana Ijumaa huko Port Louis, mji mkuu wa kisiwa hicho kilichoko katika bahari ya Hindi na kubainisha kuwa, sakata la ufisadi wa kifedha linalomsakama rais huyo limemsukuma ukutani na hana chaguo jingine ila kujiuzulu.
Amesema, na hapa tunanukuu, "Tumekubaliana na rais kuhusiana na yeye kujiuzulu na hata tarehe ya kuachia ngazi." Hata hivyo Waziri Mkuu huyo wa Mauritius alikataa kuwaambia waandishi wa habari kuhusu tarehe ya kujiuzulu rais.
Vyanzo vya habari nchini humo vimefichua kuwa rais huyo atajiuzulu rasmi Jumatatu ijayo ya Machi 12, baada ya nchi hiyo kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wake.
Port Louis, mji mkuu wa kisiwa cha Mauritius
Ameenah Gurib-Fakim, ambaye ndiye rais mwanamke pekee kwa sasa barani Afrika, anatuhumiwa kuchota fedha kutoka kwenye akaunti ya Asasi Isiyokuwa ya Kiserikali ya Planet Earth Institute yenye makao yake London Uingereza, na kutumia fedha hizo katika masuala ya kibinafsi.
Gurib-Fakim mwenye umri wa miaka 58 amekuwa rais wa kwanza mwanamke katika historia ya kisiwa hicho, tokea mwaka 2015.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG