BRELA YAWATAKA WAFANYABIASHARA KUEPUKA MIGOGORO KWAKUIGANA MAJINA
Afisa Utumishi na Utawala wa wakala wa usajili (BERLA) Raphael Mtalima wak
NA JOHN BANDA, DODOMA
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA)
imewataka wananchi kuchangamkia fursa ya kurasimisha biashara zao ili kukuza
wigo wa shughuli wanazozifanya bila kusababisha migongano ya wenyewe kwa
wenyewe unaotoka na kutumia majina yanayofanana.
Kauli hiyo imetolewa na Afisa Utumishi na Utawala
wa wakala huo Raphael Mtalima wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari
katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma ambako BRELA inashiriki kwenye wiki ya
ubunifu Tanzania MAKISATU
Afisa sheria wa BRELA Cavin Lwambogo akizungumza na wateja
Mtalima amesema wao kama wakala wanashauri kila
mfanyabiashara kuhakikisha haigi jina la mfanyabiashara mwenzake na kama
ikitokea mtu anataka kusajili jina ambalo tayari walishalisajili awali
wanamshauri mhusika kwenda kubadili jina
“mtu akija kusajili jina la kampuni na kwenye mfumo
likaonekana jina hilo lilishasajiliwa na mtu mwingine hatuwezi kumsajilia
tunamshauri aende kubalisha jina, na hapa nawashauri watu kuyatengeneza majina
yao na si kuvamia majina ya watu maana kitendo hicho na sawa na wizi au uporaji”,
Aidha amesema kwa sasa Brela inatoa elimu ya uelewa
kwa wananchi ambao wanaishi vijijini kwa kutumia vyombo mbalimbali vya habari
vya kijamii kama redia, makongamano, mikutano na maonyesho kama haya ambapo
tangu juzi tulivyoanza tunaona mwiitikio ni mkubwa kwa watu kujisajili
Afisa TEHAMA wa BRELA Joram Manyika akiwafafanulia jambo wafanyabiashara
Ameongeza amewakumbusha wafanyabiashara kuendelea
kuzihuisha kamapuni zao kila mwaka kutokana na masharti yaliyopo ambayo ni
nafuu kuliko kupitiliza mwaka na miaka bila kuzihuisha kwani watapigwa penati
za kujitakia
Amezitaja huduma zinazotolewa na BRELA kuwa ni
pamoja na usajili wa Majina ya Biashara, Usajili wa Makampuni, Usajili wa Alama
za Biashara na Huduma, utoaji wa Leseni za Biashara kundi A na Leseni za
Viwanda, utoaji wa Hataza sanjali na huduma baada ya usajili.
Kisha akazitaja sharia zinazosimamiwa na BRELA kuwa
ni pamoja Sheria ya Usajili wa Makampuni Sheria ya Usajili wa Majina ya
Biashara Sheria ya usimamizi wa Viwanda Sheria ya Alama za Biashara na Huduma
Sheria ya Usajili wa Hataza