BANDA MEDIA BLOG

No title

ASKOFU DR. CHILONGANI AWANYOOSHEA KIDOLE WANASIASA WANAOJIINUA.


Askofu Dr. Dickison Chilongani akifafanua ambo wakati akiongea na waandishi wa habari jijini Dodoma

           Na John Banda, Dodoma

           BANDA MEDIA ONE.COM

         ……………………………………………

ASKOFU wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Cetral Tanganyika na kati (DCT), Dr. Dickison Chilongani  amewataka wanasiasa waliyopo katika nafasi mbalimbali za Uongozi kujishusha ili kuondoa machafuko yanayoweza kutokea katika kipindi cha Uchaguzi Ujao wa mwaka 2025.

Dr. Chilongani ameyasema hayo leo Dec 25,2023, wakati akitoa salamu za Krismasi kwenye ibada iliyofanyika katika kanisa kuu la Roho Mtakatifu jijini Dodoma, ambapo amesema tatizo la watumishi walio wengi hupenda kujiinua kutokana na madaraka au fedha walizonazo.

Amesema mwaka 2025, kutakuwa na uchaguzi mkuu wa kuchagua viongozi wa serikali lakini chakushangaza tayari kampeni mbalimbali ni kama zimeanza, kuhusu uchaguzi huo, zimeanza kufanyika kama vile uchaguzi huo utafanyika kesho

“vitimbwi vingi vimeanza, miongoni mwa wanasiasa, wanasemana vibaya, wanachafuana, wanapigana vijembe na hata pesa zinatunamika sana, kila mtu anajiinua anajiona yeye ni bora, kila mtu anataka kuwa Rais mwaka 2025.

“hali hiyo inatokana na wanasiasa walio na viburi ambao hawawezi kujishusha kutokana na madaraka au fedha walizo nazo, wanajiinua tena wakitaka kumpita hata Rais Dr. Samia Suluhu Hassan aliyewateua katika nafasi walizonazo”, amesema

Aidha Askofu huyo amesema hivi sasa kumekuwa na Wimbi kubwa la watumishi wa Mungu ambao nao wamekua wakijiinua na hata kujifanya wao ndiyo Yesu.

“sisi watumishi wengine wa Mungu tunajiinua katika huduma tunazofanya tukitaka kumpita  hata Yesu mwenyewe, ambaye leo tunakumbuka Kuzaliwa kwake, tukisahau Yohana Mbatizaji alikuwa Nabii Mkubwa, lakini alituachia somo aliposema “mimi nipungue wewe uongezeke”, akimaanisha Yesu asilinganishwe naye katika utukufu

Alisema hayo akijua yeye hata kama angekuwa na uwezo wa kufanya chochote lakini isingekuwa sababu ya kumfanya kuwa mkubwa kuliko Bwana aliyemtuma…

Pia amewaagiza wakristo wa kanisa hilo, kuumbea uchaguzi ujao wa mwaka 2025, ufanyika vizuri, Amani iwepo na hata watu wasiweze kuchafuana.

Wakristo Duniani kote leo, Disemba 25, wamekusanyika katika nyumba za ibada kwa ajili ya kukumbuka Kuzaliwa kwa mwokozi wao Yesu Kristo, aliyezaliwa zaidi ya Miaka Elfu mbili iliyopita huko Yerusalem ya Uyahudi… 

Mchungaji Mkonde, akizungumza jambo na waandishi wa habari, mara baada ya ibada hiyo
Mchungaji Jonasy Leng'anda ambaye pia ni kasisi wa Idara ya Vijana akiwapasha jambo waandishi wa habari baada ya ibada hiyo
Mwanasiasa wa zamani aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Chilonwa Dodoma  Hezekiah Chibulunje  akipeana mikono na Mke wa Askofu Dr. Chilongani, Pendo Dickosn Mara baada ya Ibada hiyo, kuli ni Mtoto wa Mwnasiasa huyo anayeishi nchini Marekani.  

Askofu Dr. Chilongani akisalimiana na Jacob Chibulunje, ambaye pia ni Mtoto wa aliyekuwa Mbunge wa Zamani wa Jimbo la Chilonwa Mkoani Dodoma Hezekiah Chibulunje, kwa sasa Jacob Anaishi Nchini Marekani.

Mmoja wa Waumini wa Kanisa hilo Rachel Wildaf na wadogo zake wakiwa katika Picha ya Pamoja na Askofu Dr. Chilongani na Mke wa Askofu huyo Pendo Dickison, baada ya Ibada ya Krismasi 2023

Waumini mbalimbali wakisalimiana na Mke wa Askofu Chilongani walipokuwa wakitoka kwenye Ibada ya Krismasi

Baadhi ya wachungaji wa kanisa hilo wakiwa katika picha ya Pamoja na Askofu Dr. Chilongani
Waumini wa kanisa kuu la Roho Mtakatifu, Anglikana jijini Dodoma Wakifuatilia kwa makini Ibada ya Krismasi iliyoendeshwa na Askofu wa kanisa hilo Dr. Dickisoni Chilongani.

Waumini wa kanisa kuu la Roho Mtakatifu, Anglikana jijini Dodoma Wakifuatilia kwa makini Ibada ya Krismasi iliyoendeshwa na Askofu wa kanisa hilo Dr. Dickisoni Chilongani.
Waumini wa kanisa kuu la Roho Mtakatifu, Anglikana jijini Dodoma Wakifuatilia kwa makini Ibada ya Krismasi iliyoendeshwa na Askofu wa kanisa hilo Dr. Dickisoni Chilongani.
Waumini wa kanisa kuu la Roho Mtakatifu, Anglikana jijini Dodoma Wakifuatilia kwa makini Ibada ya Krismasi iliyoendeshwa na Askofu wa kanisa hilo Dr. Dickisoni Chilongani.
 



Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG