Ngema: Afrika Kusini yamuomboleza mkongwe wa 'nguzo ya utamaduni'
Mbongeni Ngema mkongwe aliyefariki Afrika Kusini. Picha/TRT Afrika.Na Charles Mgbolu
Salamu za rambirambi
zinaendelea kumiminika kwa mwimbaji mkongwe na nyota wa muziki wa Afrika
Kusini, Mbongeni Ngema, aliyefariki katika ajali ya gari huko Lusikisiki,
Eastern Cape, Jumatano akiwa na umri wa miaka 68.
Ngema alikuwa maarufu sana
kama mtunzi wa mashairi, mwongozaji, mchoraji, na mtayarishaji wa tamthilia.
Alifahamika zaidi kama mwandishi wa muziki maarufu na uliobeba tuzo, Sarafina.
"Natoa rambirambi zangu
za dhati kwa familia, marafiki, na washirika wa nguzo yetu ya kitamaduni...
Hadithi yake yenye ubunifu wa kipekee kuhusu harakati zetu za ukombozi
iliheshimu utu wa Waafrika Kusini walioteswa na kufichua ukatili wa utawala wa
kikandamizaji," aliandika Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa kwenye
mitandao ya kijamii.
Polisi wa Afrika Kusini
wanasema sababu halisi ya ajali iliyotokea saa 10:30 jioni Jumatano
haijulikani, na kwamba wanaendelea na uchunguzi.
Kazi yake kwenye filamu ya
Sarafina ilimletea teuzi tano katika Tuzo za Tony na baadaye uteuzi wenye hadhi
kubwa katika tuzo za Grammy.
Ngema alikuwa abiria katika
gari lililopata ajali
Tunzi ya ya Sarafina
ilionyeshwa kwa kwa miaka miwili Broadway, ikazunguka Marekani, Ulaya,
Australia, na Japani, na baadaye ikabadilishwa kuwa filamu.
Mchoraji maarufu wa Afrika
Kusini, Somizi Mhlongo, ambaye alifanya kazi na Ngema kwenye Sarafina, alimuita
"msanii mwenye vipaji vingi."
"Hii inauma zaidi.
Mwalimu wangu ameondoka. Mtu aliyesimama nyuma yangu na kujijengea wvipaji
vingi. Mtu wa nyuma ya sababu mimi kuwa mwenye nidhamu, mtaalamu, mwaminifu,
mnyenyekevu, mtiifu, na bidii yangu kazini..." aliandika sehemu kwenye
Instagram.
Waziri wa Sanaa na Utamaduni
wa Afrika Kusini, Zizi Kodwa, alimuelezea Ngema aliyefariki kama mmoja wa
watunzi wakubwa wa nchi hiyo.
"Pamoja na kifo cha Dkt.
Mbongeni Ngema, Afrika Kusini imepoteza mmoja wa waandishi, waandaaji wa
muziki, waandishi wa mashairi, waongozaji, na wanamuziki wakubwa. Kazi ya Dkt.
Ngema ilisherehekewa nchini Afrika Kusini na kimataifa," aliandika Kodwa
kwenye mitandao ya kijamii.
Mwigizaji maarufu wa Afrika
Kusini, Sello Maake KaNcube, pia alitoa heshima kwa shujaa huyo.
Kazi kubwa ya muziki wa Ngema
ilifanikiwa, ikiwa ni pamoja na Woza Albert, Township Fever, ambayo ilimletea
Tuzo ya Grammy (1990), Mama (1995), Asinamali (1996), Maria Maria (1997), The
Zulu – The Musical (1999), 1906 Bhambada: The Freedom Fighter, The House of
Shaka (2005), na The Lion of the East (2006).
