Uchaguzi wa DRC: Tshisekedi anaongoza huku matokeo yakiendelea kutoka
Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo siku ya Jumatatu Dec 25, ilitoa matokeo zaidi ya awali ya uchaguzi wa urais, yakiashiria kuongoza kwa kiasi kikubwa kwa kiongozi aliyeko madarakani Felix Tshisekedi.
Matokeo yaliyotangazwa na Ceni
hadi sasa yanahusu karibu kura milioni 1.9, kati ya jumla ya wapiga kura
waliosajiliwa takriban milioni 44 katika nchi kubwa ya Afrika ya kati yenye
ukubwa sawa na Ulaya ya magharibi na idadi ya watu zaidi ya milioni 100.
Ceni ilisema Tshisekedi mwenye
umri wa miaka 60, madarakani tangu 2019 na anayetafuta muhula wa pili wa miaka
mitano, alikuwa anaongoza kwa zaidi ya asilimia 81 ya kura.
Akifuata alikuwa
mfanyabiashara mashuhuri na aliyekuwa gavana wa jimbo la Katanga Moise Katumbi,
mwenye umri wa miaka 58, akiwa na kidogo zaidi ya asilimia 15% ya kura na
aliyekuwa mtendaji wa mafuta Martin Fayulu, mwenye umri wa miaka 67, akiwa na
kidogo zaidi ya asilimia 1%.
Uchaguzi Wacheleweshwa
Wapinzani wengine karibu 20, ikiwa ni pamoja na mshindi
wa Tuzo ya Amani ya Nobel mwenye umri wa miaka 68 Denis Mukwege, walishindwa
kukusanya asilimia 1%.
Ceni haijaweka wazi viwango vya ushiriki wa uchaguzi wa
Desemba 20 na 21 lakini bado inaendelea kutolea matokeo tangu Ijumaa, ambayo
yanajumuisha uchaguzi wa bunge, mkoa na wa mitaa.
Uchaguzi ulipaswa kufunguliwa Jumatano tu lakini
uliongezwa kutokana na matatizo mbalimbali ya kimkakati.
Wagombea wa upinzani walilaani "machafuko" na "udanganyifu" ambao wamedai uliharibu
'Tahadhari na Uvumilivu'
Wengine wanapanga maandamano
kwa Jumatano ijayo, wakati wengine wanatoa wito wa kufutwa kwa uchaguzi moja
kwa moja.
Askofu Mkuu wa Kanisa katoliki
Kinshasa, Kardinali Fridolin Ambongo, aliita uchaguzi huo "fujo
kubwa" wakati wa misa yake ya Krismasi Jumapili.
Kama ilivyokuwa kwa zaidi ya
balozi kumi kabla yake, kardinali alitoa wito wa "tahadhari na
uvumilivu", katika nchi masikini lakini tajiri kwa madini.
Mbali na mashaka ya wapinzani
kuhusu mchakato wa uchaguzi, kampeni imekumbwa na mgogoro mashariki, ambao
umeshuhudia ongezeko la mvutano katika miaka miwili iliyopita na kufufuka kwa
waasi wa M23.
