BANDA MEDIA BLOG

No title

WAZAZI NA WALEZI WAASWA KUTENGENEZA MASTELING BORA WA MAISHA

Padri Felix Francis Akimbatiza Moja wa Watoto hao waliobatizwa katika kigango cha Mtakatifu Ambloce Iyumbu jijini Dodoma...

 …………………………………………

NA JOHN BANDA, DODOMA

BANDA MEDIA ONE.COM   

WAZAZI na walezi wameaswa kuwalea watoto wao katika maadili mema tangu wanapokuwa na umri Mdogo badala ya kusubiri kuwakabidhi walimu wakawafundishie pindi wanapowaandikisha shuleni…

Kauli hiyo imetolewa leo Disemba 26,2023 ambayo ni siku ya Kufungua zawadi (BOXING DAY) na Padri Felix Francis wakati alipokuwa akiongoza Ibada ya Ubatizo katika Kigango cha Mtakatifu Ambloce kilichopo iyumbu Jijini Dodoma

“Steling Bora kwenye Muvi ya Maisha hutengenezwa kuanzia nyumbani, siku zote mtoto alivyo ndivyo familia ilivyo, ukiona mtoto anakata mauno hovyo kwenye michezo yake ujue wazazi hawamkemei wala kumkataza kitu”,

Amesema wazazi wasione kuwa hao ni watoto wadogo na kwamba wakiwakataza jambo ambalo wanaona ni baya basi wataonekana hawawapendi.

“hao ambao ninyi leo mnaona ni watoto mkiwaacha kufanya, kusema na kucheza kila aina ya michezo wanayo iona kwenye TV, Kesho wanapoonza shule hayohayo wanaenda kuyaonyesha kwa wenzao.

Mfano miongoni mwa wanafunzi shuleni kwangu, wakati furani nilimshuhudia mmoja akicheza mchezo wa uvunjifu kabisa wa maadili, nilipomuita mzazi wake na kumueleza akahamaki kisha akasema mbona kukata Viuno ni jambo la kawada tu, hata kwenye tv watoto wanaona”,

Padri huyo anasema ikabidi atumie Busara ya kumruhusu Yule mama aondoke, lakini kabla ya kuondoka “nikamwambia aniachae mtoto nitamfundisha na kumwekeza mwenyewe, “fikili kidogo, kama mzazi anajibu hivyo je ukimuachia mtoto kwa kumfukuza shule si ndiyo ataenda kuharibika kabisa?’’, amesema na kuoji

Aidha amesema wazazi na walezi wengine hata wakielezwa kuhusu namna ya kuwasaidia watoto wao katika malezi bora, wanakuja juu, “niwaambie sisi walimu tunajua jinsi familia zinavyoishi kupitia watoto wao, maana Nyumbani ndiko picha linapoonzia Steling hutengenezwa kuanzia nyumba”, amesema Padri huyo wa shirika la Don- Bosco ambaye kwa sasa anafanyia kazi huko mkoani Shinyanga…

Jumla ya Watoto 8, kutoka katika familia tofauti leo wamebarikiwa na kubatizwa wakikaribishwa katika kundi la washirika wa kanisa hilo ambapo wazazi, walezi na wasimamizi wao wamesisitizwa kuwa karibu nao na kwa kuwalea katika maadili ya Kikristo mpaka pale watakapokuja kujitegea wenyewe .



                                                                      Ubatizo Ukiendelea


                       kwaya ya kanisa hilo ikitoa huduma ya Wimbaji



 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG