KANISA LISILO NA NGUVU ZA KIUCHUMI LIPIGWA NA NGUVU ZA GIZA NA KUPOTEA KABISA - DR. CHILONGANI
w aumini wakiwa katika ibada hiyo
Baadhi ya waimbaji wa kwaya maarufu ya Uvuke wakiimba katika ibada hiyo
Mke wa Askofu Pendo Chilongani akisalimiana na waumini wa kanisa la Angalikana baada ya Ibada
Ibada ya mwaka mpya ikiendelea
Ibada ya Mwaka mpya wa 2024 ikiendelea
Waumini wa kanisa hilo wakifurahia jambo kwenye Ibada hiyo
Mchungaji Makonde akitoa huduma ya Meza ya Bwana kwa washirika
Askofu Chilongani akisalimiana na Mmoja wa waumini wa Muda mrefu wa kanisa hilo.
NA JOHN BANDA,
DODOMA,
BANDA MEDIA ONE.COM
.......................................................
BAADA ya Kanisa anglikana Dayosisi ya Central
Tanganyika ( DCT) kukamilisha na kuzindua jengo la Kitega Uchumi la SAFINA
lililopo Nje ya kanisa Kuu la Roho
Mtakatifu, jijini Dodoma mwaka uliopita limewataka makasisi kuanzisha miradi
katika makanisa yao.
“mwaka uliopita tulikamilisha na kuzindua Jengo la
Kitega uchumi la SAFINA, Mpango wa mwaka huu mpya wa 2024, ni kukamilisha Radio na Tv. Ili tufikishe utume wetu kwa njia ya kisasa zaidi, na makasisi wote
waliyopo katika parishi za mjini waanzishe vitega uchumi vya kujenga fremu
kwenye maeneo yao, wakishindwa baada ya mwaka mmoja nawaondoa mjini”,
Akiongea na BANDA MEDIA ONE.COM mara baada ya Ibada
ya Mwaka mpya wa 2024, Iliyofanyika
katika kanisa kuu la Roho Mtakatifu jijini Dodoma, Askofu Dr. Dickison
Chilongani amesema kanisa ili liweze kumudu kafanya huduma mbalimbali zikiwemo
za Utume, kusaidia wahitaji, Afya Elimu na kujiendesha lazima liwe na nguvu za
kiuchumi.
“sisi wakristo tunaangalia sana mambo ya kiroho
tukitaka kuhubiri na kuomba zaidi lakini tumesahau Agizo la Yesu kwenye kitabu
cha Mathayo Mtakatifu 18;19,20 la Kututaka tukahubiri injili kwa kila kiumbe na
kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi wake, sasa utawezaje kuhubiri bila kuwa na
fedha”, alisema na kuhoji
Amesema yeye anavyoamini ili kanisa liweze kutimiza
utume wake Mambo ya Kiroho na Kiuchumi yanaenda pamoja.
Aliongeza kuwa
Kanisa ambalo haliwekezi kwenye Uchumi, litatikiswa na Milango ya kuzimu na
nguvu za Giza zitalishinda na kuliangusha kabisa mwishowe litapotea kabisa na
halitaonekana tena.
Kanisa litakalodumu ni lile tu ambalo litakuwa
imara kiroho na kiuchumi ndilo litakalodumu.
Naye Mbunge wa Jimbo la Mpwapwa George Malima aliehudhuria
ibada hiyo ya kumshukuru Mungu kwa kamaliza na kuunza mwaka 2024, amesema
kanisa linapokuwa na nguvu imara za Kiuchumi, wachungaji wake hawawezi
kuombaomba
“kinachowafanya watumishi wengine kubaki
wakiombaomba ni kutokana na makanisa kukosa nguvu za Kiuchumi, hiyo ni sababu
kubwa pia ya kubuni njia za kuwatoza waumini wao ambao pia hawana kipato cha
kutosha sadaka nyingi”, amesema