BANDA MEDIA BLOG

WAKAZI WA MTAA WA ITEGA WAFANIKISHA KUCHONGA BARABARA KWA KUCHANGISHANA FEDHA BILA KUISUBIRI SERIKALI

 

Wananchi wa Mtaa wa Itega Shina namba 2 wakiangalia tingatinga lililokuwa likichonga Barabra ya Mantoga,  


Diwani wa Kata ya Nkuhungu Daid Mkandi akiwa katika picha pamoja na wakazi wa mtaa wa Mantoga wakati zoezi la kuchonga barabara ya mtaa huo likiendelea.

NA JOHN BANDA, DODOMA

WAKAZI wa Mtaa wa Itega Kata ya Nkuhungu jijini Dodoma  wamekuwa Tofauti na wakazi wa maeneo mengine hapa nchini ambao wamekuwa wakiilalamikia Serikali kuhusu maswala ya Utengenezaji wa miundombinu hasa ya barabara  ambapo wao wameamua kuchangishana fedha na kufanikisha uchongaji wa barabara yenye urefu wa mita 250.

Akiongea mbele ya Camera za waandishi wa habari katika Barabara hiyo ya Mantoga shina namba 2, leo Januari 16,2024 Ashiru Lumato ambaye ni mkazi wa mtaa huo amesema kutokana na Adha kubwa ambayo wamekuwa wakioipata ya magari kushindwa kupita kutokana na maji mengi kutuwama na kutengeneza tope la mfinyanzi waliamua kuitana wakakubaliana kisha wakaanza kuchangishana fedha kwa ajili ya kuondoa kero hiyo.

“kazi hii inayoendelea kufanyika ni nguvu zetu wenyewe, tulijikusanya wakazi wa mtaa wetu tukakubaliana kuchangishana fedha tukapata  million 2.4 na ndizo zimefanikisha zoezi hili”, amesema

Kwa Upande wake Katibu wa Shina namba 2 katika mtaa huo Asha Sengoli, amesema wakazi hao walifikia maamuzi hayo kutona na kuona kuwa kama wataisubiri serikali kuja kuwachongea barabara hiyo  watachelewa huku wao wakiendelea kuteswa na ubovu wa barabara hiyo iliyo katikati ya makazi ya watu.

Katibu mwenezi wa CCM, Tawi la Itega Zena Legu amesema wao kama chama walishirikishwa na hivyo na wao kuwaunga mkono kwa kuwachangia 150,000 kwa ajili ya kufanikisha mpango wao.

 Diwani wa Kata ya Nkuhungu Daudi Mkandi amewapongeza wananchi wa mtaa huo kwa maamuzi hayo ya ujasili na Moyo wa Kujitolea kwa Nguvu na mali zao,

“nawapongeza wananchi kwa Kuchangia Fedha na kujitolea kwa Nguvu zao katika kufanikisha zoezi hili, nimeambiwa pia kuna mkazi mmoja wa mtaa huu ni Mhandisi na ndiye aliyetoa mitambo hii ya uchongaji na magari ya kumwaga vifusi ambapo fedha zaidi ya million 2.6 zilizochangwa zimetumika kununulia mafuta

Aidha Diwani huyo aliwashauri Viongozi wa  Mitaa na Kata nyingine kuwashirikisha wananchi wa maeneo yao katika shuhuli za maendeleo  kwa kuwahamasisha badala ya kubaki wakiisubiri serikali peke yake.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG