Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara imetangaza rasmi waamuzi watakaochezesha mchezo wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Young Africans na Simba SC.
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Machi 1, 2026 katika Uwanja wa Amaan Complex, Zanzibar, kuanzia saa 2:15 usiku.
ORODHA YA WAAMUZI:
Mwamuzi wa Kati: Nassoro Mwinchui (Tanga)
Mwamuzi Msaidizi 1: Kassim Mpanga (DSM)
Mwamuzi Msaidizi 2: Hamdani Said (Mtwara)
Mwamuzi wa Akiba: Ramadhan Kayoko (DSM)
Mtathmini wa Waamuzi: Israel Mjuni (DSM)
.
Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku kila timu ikihitaji alama muhimu katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC.
.
.
Tags
MICHEZO