Nyota wa Paris Saint-Germain, David
Luiz hataki kurejea katika klabu yake kufuatia matukio ya
mashambulizi ya kigaidi Jijini Paris yaliyouwa watu 129 na kuishtua
Ufaransa na dunia nzima.
Luiz, ambaye yupo katika majukumu ya
kimataifa na timu ya Brazil, anatarajiwa kurejea Ufaransa baada ya
mchezo wa kuwania kufuzu kutinga fainali za Kombe la Dunia katika
mchezo dhidi ya Peru jumanne.
Hata hivyo beki huyo aliyesajiliwa
na Paris Saint-Germain kwa kitita cha paundi milioni 50 akitokea
Chelsea anaonyesha kusita kurejea Ufaransa kutokana na kuhofia
usalama wa familia yake na marafiki Jijini Paris.
Tags
MICHEZO KIMATAIFA

