PICHA: YANGA WALIVYOIACHA ARDHI YA BONGO KUIFATA APR
byJohn Banda-
0
Wachezaji
wa Yanga wakiwa kwenye ndege ya shirika la Rwanda Air kwa ajili ya
safari ya kuelekea Kigali nchini Rwanda kuikabili APR
Kikosi cha Yanga tayari kimeondoka jijini Dar es Salaam kuelekea
Kigali, Rwanda kwa ajili ya mchezo wa kimataifa wa klabu bingwa Afrika
dhidi ya APR utakaopigwa Jumamosi March 12, 2016.
Mabingwa hao watetezi wa taji la VPL wameondoka na ndege ya shirika la Rwanda (Rwanda Air). Wachezaji wakiingia kwenye ‘pipa’ kwa ajili ya safari ya kuelekea nchini Rwanda
Yanga inakutana na APR baada ya kuitoa kwenye mashindano timu ya Cercle de Joachim ya Mauritius. Wachezaji wakikosi cha Yanga wakiwa uwanja wa ndege muda mfupi kabla ya kuingia kwenye ndege kuanza safari
Yanga inatarajia kurejea nchini siku ya Jumapili kuendelea na ratiba ya michuano ya ligi kuu Tanzania bara 2015-16. Baadhi
ya mashabiki wa Yanga ambao wanasafiri kwa mabasi kuelekea Kigali,
Rwanda kui-support timu yao itakapokuwa ikicheza dhidi ya APR