BANDA MEDIA BLOG

No title

TAASISI YA ELIMU YA WATU WAZIMA YASHIRIKI WIKI YA UBUNIFU MAKISATU, HUKU IKIJIVUNIA KUWAPA UJUZI VIJANA AMBAO HAWAKUSOMA

kijana wa darasa la 7 akielezea kuhusu mfumo wa ulinzi unaotoa mlio pindi mlango au dirisha linapoguswa na wezi

MRATIBU wa program ya IPOSA iliyo chini ya Taasisi ya Elimu ya watu wazima nchini Dk. Sempeho Siafu ameitaka jamii kuwakusanya vijana wanaozurula mitaani bila ya kuwa na kazi maalum kwa kisingizio cha kutosoma na kuwapeleka kujifunza ufundi.

Dk. Siafu ameyasema hayo jijini Dodoma wakati taasisi hiyo ikishiriki kwenye maonyesho ya wiki ya wabunifu MAKISATU yanaendelea katika uwanja wajamhuri jijini humo

Amesema serikali imeanzisha programu hiyo inayofadhiliwa na Shirika la watoto Duniani (UNICEF) kwa lengo la kuwasaidia vijiana  kujikwamu kiuchumi na kuwaondoa katika unyonge wa umasikini

Amesema iposa ni mpango maalum ambao unachukua vijana ambao hawakuwahi kusoma na wale waliosoma shule za msingi na za sekondari ambapo wana vipaji vya ubunifu na kupelekwa shule za ufundi kupitia taasisi hiyo ya elimu ya watu wazima ambayo maombi ya kujiunga ni bure kupitia ofisi za Elimu ya watu wazima zilizopo kila mkoa

Wabunifu Musa Chengula na Frank Mselu wakimuelezea jambo kuhusu mfumo wa kuongoza magali walioubuni kwa kutumia Roboti (KUSHOTO NI MTEJA)

“wawalete sisi kwa sasa tunafundisha kisomo na  ufundi wa awali ambavyo vyote vianamsaidia mwanafunzi ambaye hakuwahi kusoma kabisa kuingia katika mfumo kwani kutokana na ubunifu lazima afike mbali

“hivi sasa tupo katika maonyesho haya na vijana hawa mnaowaona walikuja kujiunga tena kwa kuchagua fani waipendayo kama vile Umeme, uselemala, Tehama na wameweza kubuni vifaa mbalimbali kama vile Robotics, Rade security, Mathematcs Game, Motion Detetor, Securty, Trafic Light na Enqubetor”, alisema

Naye Afsa Elimu na Mratibu wa IPOSA kasulu T/c Kigoma Felician Ferdinand alisema tayari wamesha wasajili wanafunzi elfu 12 katika mikoa 9 ya Tanzania bara ambapo mwezi ujao wataifikia mikoa mingine 6 na kuwa na jumala ya miakoa 15 hivyo kuwataka vijana waliokosa kusoma kupata nafasi ya kusoma tena

"programu hii ya IPOSA iliyodhaminiwa na shirika la watoto Duniani UNICEF ni mpango utakaodumu kwa miaka 8 ukitarajiwa kuwanufaisha vijana wengi zaidi ambao walikuwa wamekata tamaa kutokana na kukosa elimu",  

Daud Yudas

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG